Ligi kuu ya NBC kuendelea hii leo kwa michezo miwili ambapo mchezo wa kuvutia utakuwa ni kati ya Wanamangushi, Coastal Union dhidi ya Azam FC mchezo ambao utapigwa majira ya saa 1:00 usiku.

Mchezo huo utapigwa katika dimba la Mkwakwani Tanga, ambapo Azam FC watakuwa wakihitaji pointi 3 muhimu hii leo baada ya kutoa suluhu kwenye mchezo wake wa ligi uliopita.
Wakati kwa upande wa Coastal Union naye anazitolea macho hizo hizo pointi tatu baada ya kutoa sare mchezo wake uliopita huku akiwa hajashinda mechi yoyote kwenye ligi mpaka sasa.
Vijana wa Dabo wanashikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi kumi na michezo minne hivyo leo hii huu utakuwa mchezo wao wa 5 ambao endapo watashinda watakaa kileleni kwenye msimamo wa ligi.

Wakati kwa vijana kutoka Tanga wao wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi wakitofautiana pointi moja pekee na anayeshikilia nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi.
Je leo hii Coastal anaweza kupata ushindi wake wa kwanza wa ligi kuu dhidi ya Matajiri wa Chamazi?

