Cody Gakpo amewataka Liverpool kuendelea kujituma huku wakipania kushinda Ligi ya Europa.

Mholanzi huyo mwenye miaka 24, alitikisa nyavu mara mbili huku Wekundu hao wakiilaza LASK 4-0 uwanjani Anfield na kujihakikishia nafasi ya kwanza katika Kundi E huku wakiwa na mchezo wa kusalia na kujikatia tiketi ya kutinga hatua ya mtoano.
Vilevile ukiachana na mpira wa miguu, Meridianbet wana michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine . Ingia meridianbet na ucheze kasino.
Luis Diaz na Mohamed Salah pia walilenga shabaha katika usiku wa kustarehesha vijana wa Jurgen Klopp.

Naye Gakpo anasisitiza kuwa wanalenga kwenda hadi fainali na kunyanyua kombe hilo kwenye Uwanja wa Aviva mjini Dublin.
Alisema: “Tunapaswa kuwa juu ya kundi kwa ubora tulionao. Lazima tuendelee kwa sababu tuna malengo makubwa ya msimu. Ni hivyo lazima tuendelee na kushinda kadri tuwezavyo. Kama nilivyosema hapo awali, tuna ubora mwingi na nadhani kwa ubora huu tunaweza kushinda michezo mingi.”
Bao la kichwa la Diaz lilifungua ukurasa wa mabao baada ya dakika 12 na Gakpo kufunga bao la kuongoza dakika tatu baadaye.

Salah alifunga kwa mkwaju wa penalti kipindi cha pili na kufikisha idadi ya mabao yake kwa Liverpool hadi 199, huku Gakpo akiongeza la nne dakika za majeruhi.
Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.
Mshambuliaji huyo aliongeza kuwa walianza vizuri lakini anadhani wangeweza kufunga zaidi. Mwishowe, ushindi mzuri. Inashangaza unapofunga kwenye Anfield, jinsi mashabiki wanavyoimba kwa kundi. Inashangaza.
Ndugu mteja usisahau kutembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000 ambapo wikendi hii mechi zipo kibao za kutosha.

Klopp alifurahishwa vile vile na kazi ya upande wake akisema kuwa mambo mengi mazuri yalitokea kwenye mchezo wa jana.
“Tulifanyia kazi safi, ambayo ndio tuliyotaka, kwa hivyo matokeo ya juu na utendaji mzuri.”

