Liverpool Wasogea Mpaka Wapili Epl

Klabu ya Liverpool imefanikiwa kufika mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza baada ya kushinda mchezo wake wa leo dhidi ya klabu ya Brentford.

Liverpool wakiwa katika dimba lao la nyumbani Anfield wameipasua klabu ya Brentford kwa mabao matatu kwa bila na kusogea mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.LiverpoolMajogoo wa Anfield sasa wamefanikiwa kufikisha alama 27 wakilingana na Man City na Arsenal ambapo City ana mchezo mmoja mkononi, Lakini Arsenal wao wanazidiwa magoli ya kufunga na kufungwa ndio maana wako nafasi ya tatu.

Vijana wa Jurgen Klopp walionekana kuutaka mchezo kuanzia dakika ya kwanza ambapo walikua wanafanya mashmbulizi langoni kwa Brentford mpaka pale ambapo walipofanikiwa kupata bao lao la kuongoza kupitia kwa Mohamed Salah.LiverpoolMohamed Salah anaendelea alipoishia kwani leo tena katika mabao matatu ya Liverpool amefanikiwa kufunga mawili na kufikisha mabao 10, Huku akiwa nyuma kwa bao moja kwa kiongozi wa mabao mshambuliaji wa Man City Earling Haaland.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.