DR Congo Waweka Historia Mpya Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Safari ya kuelekea Kombe la Dunia 2026 imechukua sura mpya baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) kuiondoa Nigeria kwenye hatua za mchujo kwa ushindi wa mikwaju ya penalti. Katika mchezo uliopigwa Rabat, Morocco, Wacongo walionyesha ubora wa hali ya juu na kushinda 4–3 kwenye mikwaju ya penalti baada ya sare ya 1–1 ndani ya dakika 120.

Nigeria, waliokuwa wanaonekana bora kwenye makaratasi kutokana na nafasi yao ya juu kwenye viwango vya FIFA, waliingia kwa kasi na kupata bao la mapema kupitia shuti la Frank Onyeka lililomgonga Axel Tuanzebe na kumuacha kipa Lionel M’Pasi. Hata hivyo, DR Congo hawakuruhusu bao hilo la mapema kuwaangusha.

DR Congo Waweka Historia Mpya Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Walipanga upya mchezo wao, wakatafuta nafasi na hatimaye Mechak Elia akasawazisha dakika ya 32 baada ya uzembe wa nahodha wa Nigeria, Wilfred Ndidi, kwenye eneo la hatari. Kuanzia hapo, upepo wa mchezo uligeukia upande wa Wacongo.

Kadri dakika zilivyozidi kusonga, DR Congo walionekana kujiamini zaidi, hasa baada ya Nigeria kumpoteza mshambuliaji wao hatari Victor Osimhen kutokana na majeraha mwishoni mwa kipindi cha kwanza. Kasi ya Wacongo iliwalazimu Nigeria kucheza kwa tahadhari, lakini bado iliwacharaza jasho kwenye dakika ya 83 baada ya makosa ya kipa Stanley Nwabali yaliyokaribia kuwamaliza.

Katika dakika za nyongeza, DR Congo walidhani wamepata bao la pili, lakini mwamuzi wa Morocco akalikataa kwa madai ya faulo kabla ya mfungaji Noah Sadiki kumalizia mpira wavuni.

DR Congo Waweka Historia Mpya Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kipindi cha penalti kiligeuka kuwa tamthilia ya ushujaa. Kocha wa DR Congo alifanya uamuzi wa kifundi kumtoa M’Pasi dakika ya mwisho ya muda wa ziada na kumuingiza Timothy Fayulu, uamuzi uliolipa baada ya kipa huyo mpya kuokoa penalti mbili muhimu.

Kwa ushindi huo, DR Congo sasa watashiriki mashindano maalum ya mchujo wa mabara sita yatakayofanyika Guadalajara na Monterrey, Mexico mnamo Machi 2026. Watakuwa miongoni mwa mataifa sita yatakayowania tiketi mbili za mwisho kuelekea Kombe la Dunia.

DR Congo Waweka Historia Mpya Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Hadi sasa, Bolivia na New Caledonia tayari wameshafuzu play-offs hizo, huku mataifa kutoka Asia, CONCACAF na Oceania yakihitimisha safari zao za kufuzu wiki hii. Timu mbili zenye viwango vya juu zaidi zitapata nafasi ya moja kwa moja kucheza fainali za mchujo, huku nne zikipambana kwenye nusu fainali moja kwa moja.

Kombe la Dunia 2026, litakaloshirikisha timu 48 kwa mara ya kwanza katika historia, litafanyika Marekani, Canada na Mexico. Afrika tayari ina mataifa tisa yaliyokata tiketi moja kwa moja: Algeria, Cape Verde, Misri, Ghana, Ivory Coast, Morocco, Senegal, Afrika Kusini na Tunisia.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.