Manchester United Yaanza Majadiliano ya Ndani Kumtafuta Kocha wa Kudumu

Klabu ya Manchester United FC imeanza kuongeza kasi katika mchakato wa kutafuta kocha mpya wa kudumu, huku mustakabali wa kocha wa muda Michael Carrick ukiendelea kuwa haueleweki ndani ya klabu hiyo

Ingawa Carrick bado anaungwa mkono katika nafasi yake ya sasa, taarifa kutoka ndani ya klabu zinaeleza kuwa uongozi wa United umefikia hatua muhimu ya kupanga mustakabali wa benchi la ufundi baada ya msimu huu kumalizika.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Manchester United Yaanza Majadiliano ya Ndani Kumtafuta Kocha wa Kudumu

Baada ya mchezo wao dhidi ya AFC Bournemouth uliopangwa kufanyika Machi 20, United haitacheza tena hadi Aprili 13, kipindi ambacho kinatajwa kuwa muda muhimu kwa viongozi wa klabu kuanza majadiliano ya kina kuhusu makocha wanaoweza kuinoa timu hiyo.

Manchester United Yaanza Majadiliano ya Ndani Kumtafuta Kocha wa Kudumu

Ripoti zinaeleza kuwa kocha wa timu ya taifa ya Germany, Julian Nagelsmann, ni miongoni mwa majina yanayowavutia viongozi wa Manchester United, huku klabu ikitarajiwa kufanya mawasiliano ya awali ili kujua kama angekuwa tayari kujiunga na timu hiyo siku zijazo.

Manchester United Yaanza Majadiliano ya Ndani Kumtafuta Kocha wa Kudumu

Kocha mwingine anayefikiriwa ni Roberto De Zerbi ambaye kwa sasa hana timu, ingawa United haijakata tamaa ya kuwafuatilia hata makocha ambao tayari wanafanya kazi katika vilabu au timu nyingine endapo wataona kuna nafasi ya kuwapata.

Manchester United Yaanza Majadiliano ya Ndani Kumtafuta Kocha wa Kudumu

Licha ya Carrick kufanya kazi nzuri hadi sasa na kuiweka United katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Premier League, uongozi wa klabu bado unaendelea kuchunguza chaguo mbalimbali kwa ajili ya mpango wa muda mrefu, hasa baada ya kichapo cha hivi karibuni dhidi ya Newcastle United FC kuonyesha kuwa timu hiyo bado inahitaji maboresho zaidi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.