Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF) limefanya mabadiliko makubwa kwenye benchi la ufundi la timu ya taifa kabla ya FIFA World Cup 2026 itakayoanza Juni 11 hadi Julai 19, 2026. Mohamed Ouahbi ametangazwa rasmi kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Morocco, mara tu ya kujiuzulu kwa kocha wa zamani, Walid Regraguihapo jana.

Kuondoka kwa Regragui kunafuata baada ya Morocco kushindwa kushinda Africa Cup of Nations 2025 walipoikaribisha kwenye uwanja wao. Morroco walifika fainali lakini walipoteza 1-0 dhidi ya Senegal katika mchezo uliojaa utata uliofanyika Rabat Januari 18, 2025.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
FRMF imeeleza wazi kuwa Ouahbi, aliyewahi kuwa kocha wa vijana wa Anderlecht, ataiongoza Morocco kwenye Kombe la Dunia akiwa na Joao Sacramento na Youssouf Hadji kama wasaidizi wake. Ouahbi aliiongoza timu ya vijana ya Morocco U-20 kushinda Kombe la Dunia la vijana chini ya miaka 20 mwaka 2025 nchini Chile, akishinda fainali dhidi ya Argentina 2-0, akipatia Morocco taji lao la kwanza la kihistoria.


Ouahbi ana historia ya muda mrefu katika soka la vijana, akianza kuinoa akiwa na umri wa 21, na kupandishwa hadi kuinoa timu za U10 hadi U21 Anderlecht kabla ya kuchukua timu ya taifa ya U-20 ya Morocco. Tuzo ya Kocha Bora wa CAF mwaka 2025 pia ilimnukuu kutokana na mafanikio yake makubwa.

Ouahbi sasa anatarajiwa kuendeleza mafanikio hayo na kuiongoza Morocco katika Kombe la Dunia la 2026, huku shabiki na wachezaji wakitarajia uongozi wake uliothibitisha matokeo makubwa ya kihistoria.


