Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, limetangaza kuufungia matumizi uwanja wa Sokoine uliopo Mbeya kwa michezo ya ligi kutokana na kukosa vigezo vinavyotakiwa kikanuni na kisheria katika miundombinu ya mpira wa miguu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo, miundombinu ya uwanja huo haikidhi matakwa ya kanuni kama ilivyoainishwa katika masharti ya Kanuni za Leseni za Klabu. Kutokana na hali hiyo, TFF imechukua uamuzi wa kuufungia uwanja huo hadi pale marekebisho yatakapofanyika na kupitishwa na shirikisho hilo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kutokana na uamuzi huo, timu ambazo hutumia uwanja Sokoine kwa michezo yao ya nyumbani zitalazimika kutumia viwanja mbadala kwa muda hadi pale maboresho yatakapokamilika na kuruhusiwa tena na Tanzania Football Federation. TFF pia imezikumbusha klabu zote nchini kuendelea kutunza na kuboresha miundombinu ya viwanja ili kukidhi matakwa ya kanuni za mpira wa miguu.


