Osimhen, Nwabali Wakosekana Kikosi cha Nigeria kwa Mechi za Kirafiki

Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Eric Chelle, ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kitakachoshiriki mashindano ya kirafiki ya mataifa manne mwezi huu, huku nyota Victor Osimhen na kipa Stanley Nwabali wakikosekana kwenye orodha hiyo.

Osimhen, Nwabali Wakosekana Kikosi cha Nigeria kwa Mechi za KirafikiNigeria, mabingwa mara tatu wa Afrika, ambao walimaliza katika nafasi ya tatu kwenye AFCON 2025 iliyofanyika Morocco, wanatarajiwa kushiriki michuano hiyo pamoja na timu za taifa za Iran, Jordan na Costa Rica.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa  

Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Nigeria, mashindano hayo ni sehemu ya mpango mpana wa kiufundi wa kuimarisha timu ya taifa kuelekea mashindano yajayo. Kikosi hicho kimejumuisha majina makubwa kama Ademola Lookman, Maduka Okoye, Akor Adams, Frank Onyeka, Igoh Ogbu pamoja na wachezaji wa Fulham akiwemo Alex Iwobi na Calvin Bassey.

Osimhen, Nwabali Wakosekana Kikosi cha Nigeria kwa Mechi za KirafikiKutokuwepo kwa Nwabali kunaelezwa kuchangiwa na hali yake ya kutokuwa na klabu kwa sasa baada ya kuvunja mkataba na timu ya Chippa United. Hali hiyo imewapa nafasi makipa Francis Uzoho na Adebayo Adeleye kujumuishwa kikosini.

Kwa mujibu wa ratiba ya mashindano hayo, Jordan wataanza kampeni yao dhidi ya Costa Rica Machi 27, huku Iran wakicheza na Nigeria siku hiyo hiyo. Siku nne baadaye, wenyeji watacheza dhidi ya Nigeria wakati Iran wakimalizia ratiba yao kwa kuvaana na Costa Rica.

Osimhen, Nwabali Wakosekana Kikosi cha Nigeria kwa Mechi za KirafikiKatika kikosi hicho, makipa walioteuliwa ni Maduka Okoye, Adebayo Adeleye na Francis Uzoho. Mabeki ni Calvin Bassey, Semi Ajayi, Bright Osayi-Samuel, Bruno Onyemaechi, Zaidu Sanusi, Igoh Ogbu na Emmanuel Fernandez.

Osimhen, Nwabali Wakosekana Kikosi cha Nigeria kwa Mechi za KirafikiViungo ni Alex Iwobi, Frank Onyeka, Wilfred Ndidi, Raphael Onyedika na Fisayo Dele-Bashiru, huku washambuliaji wakiwa Ademola Lookman, Samuel Chukwueze, Moses Simon, Chidera Ejuke, Paul Onuachu, Akor Adams, Philip Otele na Collins Yira Sor.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.