Neymar ametawala vichwa vya habari toka dirisha la uhamisho lilipofunguliwa. Nyota huyu amekuwa akitamani kuondoka klabuni PSG na kurejea klabu yake ya zamani ya Barcelona.
Hata hivyo, suala la uhamisho wa staa huyu limekuwa na dana dana nyingi huku kikwazo kikubwa kikitajwa kuwa ni dau kubwa.
Barcelona walitajwa kufanya mazungumzo na klabu ya PSG, na mpaka sasa wanatarajiwa huenda likatokea jambo kabla ya dirisha la uhamisho kufungwa.
Kwa upande mwingine, Real Madrid nao walikuwa wanaimezea mate sahihi ya staa huyu. Dau la staa huyu linaonekana kutokuwepo kwabisa kwenye mipango ya manunuzi ya klabu hiyo, kama ambavyo waliamua kutemana na Pogba.
Taarifa za hivi punde, kwa mujibu wa L’Equipe zimetaja kuwa Neymar ameamua kuwaambia klabu ya PSG kuwa atasalia klabuni hapo baada ya kushindikana kwa uhamisho kuelekea klabu ya Barcelona.


isha
Neymar usiondoke bhuanaa
Furahav
Aende tu.
Povel
Gud update