Paulo Dyabala atalazimika kuendelea kusalia karantini, hata ikiwa mazoezi yataanza karibuni. Staa huyu bado anaendelea kupambana na virusi vya corona ambavyo alithibitishaa kuwa navyo.
Baada ya wachezaji wenzake wawili hivi karibuni kupimwa na kupimwa na kukutwa bila maambukizi, Juventus walitangaza mshambuliaji huyu Muargentina alipatikana na maambukizi katika vipimo vilivyofanyika Tarehe 21 Machi.
Kwa mujibu wa ripoti ya Sysport, nyota huyu ameendelea kukaa Karantini nyumbani kwake. Dybala bado hajaweza kupona kabisa virusi vya corona toka aliporipoti kuwa yeye na mpenzi wake walikuwa wameambukizwa virusi hivyo.
Juventus ilikuwa ni klabu ya kwanza wa wachezaji wake kujitokeza kutangaza kuwa wamepata maambukizi ya virusi vya Corona. Dyabala alikuwa mchezaji wa pili, baada ya Daniel Rugani kuthibitika amepata maambukizi. Blaise Matuidi pia alipatikiana na maambukizi, lakini yeye na Rugani wameshapona kwa sasa.
Hata hivyo, nyota huyu anaendelea vizuri na anaonekana kuwa na afya isipokuwa hajaweza kurejea hali ya kutokuwa na virusi kabisa.
Ratiba rasmi ya kurejea kwa Ligi ya Serie A bado haijapatiwa majibu wakati serikali ikiwa inatarajiwa kutoa muongozo zaidi siku za hivi karibuni. Kuna matumaini kuwa Ligi inaweza kuendelea mapema mwezi mei.


Tatu fikirini
Poa tu
SADICK
Asante Meridianbet kwa taarifa hizi muhimu
Winfrida mpanda
Mungu atamsaidia atapona na kuendelea na mazoezi
Samiah
Habari zakusikitisha hizi
Antony Luseno
Ni jambo la kheri endapo kama anaendelea vizuri maana ligi ikirejea Juve itamhitaji sana
WAZIRI SHOMARI
Ahsante meridianbet kwa kutujuza
Zainabu kihongosi
Mungu asaidie awe imara tunahitaji ligi iendelee
Wahida
Ohoool so sad Corona🦠virus big problem
Ernest Kimeru
Get well soon Dybala!! keep fighting>>>
Mwajuma
Mungu amsaidie awe na afya njema
Ester jackson
Mungu amfanyie wepesi mana bado nikiungo muhimu katika timu
Abram
Mungu atamsaidia atakuwa pouwa soon mpaka ratiba rasmi ya Ligi ya Serie A ikifikia kurejea serikali ikitoa muongozo mambo yote yatakuwa sawa tuwe na matumaini mpaka mwezi mei ligi ikiendelea mambo yatakuwa fresh jamaa anaweza kuwa fresh🙏🏽
Frank patrick
Dybala10 soon atakuwa sawa
Gabriel
Bad news kwa kiungo huyo club ila jambo la msingi kuomba apone
Neema Juma
Mungu amsaidie kwa kweliii
Hidaya Mohammed
Mwenyezi mungu amfanyie wepesi arudi kwenye afya yakel
Schola
Corona daah imemuharibia sn
Neema hassan
Mungu amsaidie apone bado tunamhitaji kiungo wetu..
aisha
mungu amsaidie apone
Adelta
Mungu amsaidie apone
Rehema
Pole Sana jembe mungu akusaidie
Rehema
Pole Sana jembe mungu!
Elika
Inshallah mwenyezi mungu awafanyie wepesi inshallah
Dorophina
Corona mungu amsaidie apone arudi tena ulingoni
farida ahmadi
Paul dyabala afya ni bora Mungu atakujaalia tyuu hutapona na mashabiki wako tunakusubiri