Mchezaji Bora Kutoka Uholanzi Ndani ya EPL

Hivi umeshawahi kujiuliza ni mchezaji gani kutoka Uholanzi anafanya au alifanya poa sana ndani ya ligi kuu ya Uingereza, EPL? Bergkamp? Hasselbaink? Van Nistelrooy?

Kumekuwa na wachezaji waliobarikiwa ndani ya Premier League na unapotaja hao wachezzaji huwezi kukosa kuwataja wale waliopo huko wakitokea Uholanzi.

Mafanikio ya juu kisoka kufikiwa ndani ya EPL imejumuisha wachezaji kadha wa kadha kutokea Uholanzi. Jumla ya Waholanzi 133 wamecheza kandanda la kulipwa ndani ya Premier League tangu pale Hans Segers na Michel Vonk walipoingia kuchezea timu za Wimbledon na Manchester City katika ufunguzi wa msimu mpya wa Premier League miaka hiyo.

Baadhi wamekuwa watata sana uwanjani na wamekuwa wabunifu mno wakati wengine wakizipatia ulinzi mkubwa timu zao walizozitumikia kisoka.

Washambuliaji watatu kutokea Uholanzi wameshinda Golden Boot, ambapo akina Jimmy Floyd Hasselbaink na Robin van Persie wote hao wamenyakua tuzo hizo mara mbili na mwingine Ruud van Nistelrooy aliongoza katika takwimu ya wafungaji mabao wa msimu wa 2002/03 na pia akashinda tuzo ya Player of the Season.

Dennis Bergkamp anashikilia rekodi ya Premier League kwa kuongoza katika kutoa pasi za magoli kwenye mechi alizocheza, amesaidia upatikanaji wa magoli manne kwa Arsenal dhidi ya Leicester City mwezi Februari mwaka 1999.

Na katika upande mwingine wa uwanja, Edwin van der Sar ana rekodi kubwa sana ya kwenye upande wa clean sheets, anazo 14 jumla na ni kwa mfululizo kwa klabu ya soka ya Manchester United katika msimu wa 2008/09 wa EPL.

Ameweka clean sheets 132, hizo ni mara 86 zaidi ya kipa yeyote kutokea Uholanzi.

Angalia hapa namba zinazoongoza kwenye PL kwa wachezaji wa Uholanzi

Mechi Magoli Pasi za Mabao
George Boateng 384 Robin van Persie 144 Dennis Bergkamp 94
Dennis Bergkamp 315 JF Hasselbaink 127 JF Hasselbaink 58
Edwin van der Sar 313 Ruud van Nistelrooy 95 Robin van Persie 53
JF Hasselbaink 288 Dennis Bergkamp 87 Dirk Kuyt 27
Mario Melchiot 284 Dirk Kuyt 51 Marc Overmars 19

 

Van der Sar alifuata nyayo za mwenzake kutoka taifa moja, Jaap Stam, ambaye aliwika sana kwa klabu ya Man Utd kati ya miaka ya 1998 na 2001, akishinda taji kwenye misimu yake yote mitatu akiwa pale Old Trafford.

Kuna beki wa kati kutoka Uholanzi aliyewika na kuweka hatari sana katika misimu miwili iliyopita, huyu si mwingine bali ni Virgil van Dijk aliyeitumikia vyema sana klabu ya soka ya Liverpool na kufanikiwa kushinda tuzo ya Player of the Season msimu wa 2018/19.

Angalia takwimu hizo zinazovutia kwenye jedwali hapo juu kuweza kuona namna Waholanzi walivyofanya poa sana Uingereza. Kwako wewe unadhani ni nani anastahili kuwa mchezaji bora zaidi kutoka Uholanzi?

18 Komentara

    Robin Van Persie was great striker

    Jibu

    Mchezaji Bora alikuwa Ni van nistelrooy alikipiga Sana

    Jibu

    George boateng

    Jibu

    Bergkamp alikuwa hatar ktk assist

    Jibu

    Namkubali sanaaaa huyo

    Jibu

    Robin jamanii nikimuona natamani Mpira usiishe

    Jibu

    Robin van persie alikuwa na kipindi au msimu mzuri hasa baada ya kupona majeraha yake ya mara kwa mara ila dennis bergkamp ni mchezaji bora wa muda wote kwenye premier

    Jibu

    Salute kwa Dennis Bergkamp!!¡!

    Jibu

    Mario melchiot ni noumaaaa

    Jibu

    Namkubali Sana Mario melchiot

    Jibu

    Van Nistelrooy Alifanya bia sana

    Jibu

    Robin van persie yuko vizuri sana kuliko wengine

    Jibu

    Uholanzi wanatisha sana

    Jibu

    Hao ni wachezaji moto wa Uholanzi..Asante Meridinbet kwa taarifa

    Jibu

    Legends

    Jibu

    Hn mpinzan hyo

    Jibu

    Uholanzi wako vzur

    Jibu

    Van persie mwamba

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.