Chelsea Watamuachia Kepa kwa Donnarumma?

Ripoti zinazochanja mbuga kwa kasi kule Uingereza ni kuwa klabu ya Chelsea inataka kufanya dili la mabadilishano kati ya mlinda mlango wake Kepa Arrizabalaga ili kumpata golikipa Gianluigi Donnarumma wa Milan.

Mkataba wa sasa wa mzuia mikwaju Donnarumma pale San Siro unaisha mwaka 2021, na kwa mujibu wa wakala wake Mino Raniola mpaka sasa hakuna maongezi yaliyofanyika kumuongezea mkataba.

Sababu ya kutofanyika kwa mazungumzo ya kusaini mkataba mwingine inatajwa kuwa ni kwa sababu klabu ilikuwa ‘bize’ na suala la mkataba la Zlatan Ibrahimovic, mazungumzo ambayo yamekamilika wikiendi hii na dili linatarajiwa kuwa litasainiwa Jumatatu.

Bada ya ishu ya Zlatan, sasa Milan wanaweza kurejea kwa Donnarumma kuhakikihsha kuwa hataondoka kama mchezaji huru msimu ujao.

Hata hivyo, taarifa zinataja kuwa klabu ya Chelsea ilikuwa inafanya mazungumzo na Donnarumma, na wapo tayari kumtoa Kepa na kiasi cha pesa ili kumnasa golikipa huyu mwenye miaka 21.

Kepa ambaye sasa anatimiza miaka 26 Oktoba, alinunuliwa kwa €80m katika msimu wa joto wa mwaka 2018, lakini hivi karibuni amekuwa akiachwa kikosini kwa sababu ya makosa kadhaa.

Hata hivyo, vyanzo vya habari vya Italia havizungumzii kwa upana suala hili. Inawezekana Milan wakahitaji kusalia na Donnarumma.


 

Beti Mbio za Mbwa Mubashara

Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.

Cheza Hapa

36 Komentara

    Asante kwataharifa

    Jibu

    Kama nivyo nivizuri mwendo wakupiga pesa tuu hapo

    Jibu

    Hilo bonge la dili la maana kwa klabu hizo mbili

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Hapana Kepa ni level nyingine..

    Jibu

    chelsea wakisema wamtoe kepa watakuwa wamekosea sana maana kepa ana msaada mkubwa sana pale

    Jibu

    Asanteni meridianbet kwa taarifa nzuri

    Jibu

    habar njema

    Jibu

    Itakuwa powa sana kama chelsea wakimpata Gianluigi donnarumma wa milan

    Jibu

    Kama kepa kashafungashiwa virago the blues

    Jibu

    Hii ni fursa kwa wakala mwenye makeke mengi Mino Raiola kutengeneza pesa kama kawaida yake, sidhani kama AC Milan itakuwa tayari kumupoteza golikipa wao namba moja#meridianbettz

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Inawezaka tu

    Jibu

    Chelsea kwa sasa kiu yao kubwa ipo kwa mlinda mlango ipo tayari kufanya lolote kupata mlinda mlango mwengine kwa ajiri ya msimu ujao.

    Jibu

    Dah saiv wanatak kumtoa chambo

    Jibu

    Wafanye chaguo sahihi maana hawachelewi lawama kurudisha kwa kipa!!!

    Jibu

    Kama hili dili likikubaliwa na Milan basis Chelsea watakuwa wameokota dodo kwenye mnazi .

    Jibu

    Hahahaha Chelsea wamemchoka kipa wao arrizabalagakama man u walivyomchoka de gea kwa kufungwa magoli ya kizembe

    Jibu

    Milan wasijiroge kumuachia golie wao

    Jibu

    Gud newz

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    dili la maana

    Jibu

    Utoto umemponza Kepa na tamaa ya kuwa bora ghafla bila kujifunza zaidi kutoka kwa wakongwe, Binafsi namuona kama kipa hodari tena kijana sema anatakiwa kujifunza kitu juu ya nidhamu na kujenga kitu kinaitwa team work katika maisha yake ya soka.

    Jibu

    Asantee kwa taarifa

    Jibu

    Iko poa

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Wasimuache kepa

    Jibu

    Chelsea wajitahidi wampate atawafaa

    Jibu

    Habar njm

    Jibu

    Chelsea kama wakipata saini ya mlinda mlango huyo tayali watakua washaimarisha kikosi chao so tumeona kwenye usajiri wao wamefanya vizuri sana

    Jibu

    Dili bomba

    Jibu

    Chelsea wangemchukua huyu ingekuwa poa sana

    Jibu

    Chelsea kwa sasa kiu yao kubwa ipo kwa mlinda mlango ipo tayari kufanya lolote kupata mlinda mlango mwengine kwa ajiri ya msimu ujao.

    Jibu

    fursa kwa wakala mwenye makeke mengi Mino Raiola kutengeneza pesa kama kawaida yake, sidhani kama AC Milan itakuwa tayari kumupoteza golikipa wao

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.