Jeremie Boga Kuwanufaisha Chelsea

Klabu ya Chelsea ipo mbioni kupata kiasi kikubwa cha fedha kupitia Jeremie Boga iwapo kiungo huyu nyota wa kikosi cha Sassuolo atauzwa.

Nyota huyo wa Sassuolo anahusishwa na dili la kusajiliwa na timu ya Ufaransa ‘Rennes’ ambayo imeweka mezani ofa ya pauni 17m ili kunasa saini ya nyota huyo.

Mkurugenzi wa Chelsea, Marina Granovaskaia alifanikiwa kuweka kipengele kinachowawezesha Chelsea kupata 15% ya ada yoyote ambayo mchezaji huyo wa zamani wa Chelsea atasajiliwa na timu nyingine.

Jeremie Boga (23), aliyekuwa na mafanikio makibwa katika misimu miwili iliyopita, anawaniwa wa vilabu vya Napoli, Roma na Atalanta lakini Rennes ndiyo wapo karibu zaidi kupata saini ya nyota huyo.

Nyota huyo ambaye ni zao la kituo cha kukuzia vipaji cha Chelsea, amejipatia uzoefu mkubwa mara baada ya Chelsea kumpeleka kwa mkopo katika vilabu mbali mbali vya ligi za La Liga, Championship na Ligue 1 kabla hajaamua kuihama mazima klabu hiyo ya London mwaka 2018.

Kwa upande wa Boga mwenyewe, yupo tayari kwenda kutafuta changamoto sehemu nyingine nje ya Sassuolo na Rennes ndiyo panapoelekea kuwa kituo chake kinachofuata.

Kocha wa Rennes, Julien Stephan ameweka wazi kuwa anavutiwa na mchezaji huyo wa Sassuolo na yupo tayari kumsajili.

“(Jeremie Boga) ana uwezo mkubwa wa kukaa katika nafasi, kutengeneza na kumalizia mashambulizi. Ninamfahamu vema kwa kuwa alishaichezea timu hii kwa mkopo misimu michache iliyopita. Mimi na yeye tunafahamiana, japo kipindi hicho nilikua nafundisha kikosi cha pili cha timu hii.”

Katika hatua nyingine, kaka wa Boga, ambaye pia ni wakala wake, amesema kuwa Boga anawaniwa na timu nyingi za Seria A na EPL lakini maamuzi juu ya wapi atakwenda ni juu yake mwenyewe.

Kwa upande wa Chelsea wenyewe, watapata 15% ya ada ya usajili itakayotolewa na klabu yoyote itakayomsajili Boga.

 


 

SHINDA NA HI LO

Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.

Cheza Sasa

40 Komentara

    Hongera

    Jibu

    bonge moja la dili likikamilika chelsea hawatakuwa na njaa tena

    Jibu

    Bonge la dili kwa Chelsea wakifanikiwa kumuuza mchezaji wao

    Jibu

    Iyo ndo faida team kukuza vipaji baadae km ivi inaleta kweny team pale anapouzw

    Jibu

    Ilo ni dili kubwa kwa chelsea wakifanikisha hakika watatusua sana#Meridianbettz

    Jibu

    Hongera sana kwake

    Jibu

    Dili limekaa powaaa!

    Jibu

    Anastahili kupewa pongezi
    @meridianbettz

    Jibu

    Hapa faida inaingia kote Chelsea na kwa Sassuolo

    Jibu

    Mambo ya pesa ayo

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Bonge ladiri Chelsea pesa Zina wanukia

    Jibu

    Pesa ndio mpango mzima

    Jibu

    bonge moja la dili

    Jibu

    Hongera sana kwake

    Jibu

    Kwenye pesa hakuna kinachoshindikana

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Safi sana Chelsea bonge la dili

    Jibu

    Dili limekaa poa#meridianbettz

    Jibu

    Deal done

    Jibu

    Wenzetu hapa wanachezaga sana hapa wanajua kupiga hela kupitia mikataba

    Jibu

    Hongera sana

    Jibu

    Hongera sana kijana

    Jibu

    Dili limetiki

    Jibu

    Ndo faida ya kulea vipaji saf

    Jibu

    Bongee la dilii hilo

    Jibu

    Hongera yake

    Jibu

    Kibiashara zaidi pesa mbele mengine baadae!!!

    Jibu

    Hongera

    Jibu

    Big up broh

    Jibu

    Chelsea wamekua wajanja Sana kwenye vipengele vya wachezaji kwenye mikataba yao hili lilionekana pia kwenye kipengele cha Edin hazard.

    Jibu

    Hapana chezea hela na Chelsea wako vizuri kwa ujumla na hela mana hapo ni dili kubwa sana la kuwaingizia hela Chelsea pia tukumbuke kuwa pia kunamchezaji ambaye anaingizia timu hiyo hazard ambaye anaichezea real Madrid

    Jibu

    Safi

    Jibu

    The blues wanafaidika kwa vipaji vyao

    Jibu

    💪

    Jibu

    Mkurugenzi Marina Granovaskaia amekuwa na mbinu wa kuweka vipengele vinavyoinufaisha Chelsea baadaye#meridianbettz

    Jibu

    Pesa ndio mpango mzima

    Jibu

    Unaambiwa pesa inaongea

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.