Klopp na Utaalamu wa Kuendesha Gari Bovu Alilolizoea

Liverpool hawajafanya maingizo yoyote mapya kwenye kikosi chao zaidi ya Kostas Tsimikas, beki wa kushoto kutoka Ugiriki, si usajili unaofikirisha. Tunajua anakuja kumsubiri Andy Robertson, ila si kuingia kwenye kikosi cha kwanza.

Bado ukisoma magazeti kutazama tetesi za usajili, Liverpool wao hawapo. Taarifa yao ni moja tu, Thiago Alcantara, hakuna mwingine na dili la Alcantara litafanikiwa tu iwapo Giorgio Wijnaldum atajiunga na Barcelona.

Hii inamaanisha nini? Klopp anaamini anaweza kwenda kutetea taji lake na kikosi kilekile kilichotwaa taji msimu uliopita. Ndiyo maana hajihangaishi sokoni. Swali linakuja, Je ni kweli Liverpool wanaweza kutetea taji na kikosi kilekile?

Kwa haraka, akilini kwetu ni kitu kisichowezekana, haswa tukitazama usajili walioufanya Chelsea na Man City. Zaidi ya yote, tunaamini Liverpool wamechoka, wametumia kikosi hichohicho kwa miaka mitatu. Watasumbuliwa na ‘fatigue’ na kisaikolojia hawapo kimapambano. Kwanini? Walifika fainali ya UEFA, msimu uliofuata wakachukua, wakawa wa pili kwenye ligi, msimu uliofuata wakachukua ligi. Unadhani wanahitaji nini tena? Hakuna. Hivo hawawezi kuwa na ari kama waliyokuwa nayo misimu mitatu nyuma.

Hizi ni hoja za msingi, tena zina mashiko. Ila nilikuwa na mawazo tofauti kidogo. Mimi binafsi yangu, ninaamini Liverpool wanaweza kulitetea taji lao. Kwanini?

Kwanza sidhani kama Liverpool inahitaji sura mpya sana. Sioni eneo ambalo Liverpool wana udhaifu. Kuanzia golini mpaka mbele. Liverpool wanakosa kikosi kipana tu, ila hawakosi wachezaji bora. Isitoshe Minamino na Keita hawakutumika msimu ulioisha, uwepo wao ni sawa na usajili mpya.

Pia wachezaji wengi wa Liverpool wapo katika umri wa kuwa kwenye peak. Tukimuacha TAA mwenye miaka 21. Wengi wapo katika umri wa kuwa kwenye moto. Hili linatokea wakiwa wamecheza pamoja kwa muda mrefu. Hawahitaji muda tena kuzoeana.

Mwisho tusisahau kuwa kocha wao ni Jurgen Klopp. Mtu aliyefanya visivowezekana viwezekane. Aliifikisha Dortmund mbovu fainali ya UEFA, akachukua nayo Bundesliga. Ameigeuza Liverpool kuwa tishio kwa mikakati tu. Tusisahau huyu ni Klopp.


SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

38 Komentara

    Ni kweli kikos cha liverpool siyo kibaya.hadi kocha wao chamsingi wachezaji wajipange vizuri msimu mpya#meridianbett

    Jibu

    Hapa kazi ipo tusubiri tuone@meridianbettz

    Jibu

    Klopp anajiamini na kikosi chake kwamba kinaweza kumletea tena ushindi msimu huu unaoanza

    Jibu

    Klopp anaamini anaweza kutetea tena taji lake kwa kikosi kile kile

    Jibu

    Liverpool bado wana timu kubwa sana ambayo haihitaji marekebisho makubwa vinginevyo labda kuwe na mchezaji anataka kununuliwa

    Jibu

    Klopp anaamini anaweza kutetea

    Jibu

    Klopp yupo vizuri sana

    Jibu

    Klopp aliimarisha Liverpool kwa awamu ,msimu ulipoisha aliangalia pengo lipo wapi na kufanya usajiri kulingana na mahitaji#meridianbettz

    Jibu

    Klopp anajiamin sana na kikosi chake#Meridianbettz

    Jibu

    Hii inamaanisha klopp anawaamini wachezaji wake

    Jibu

    Klopp yup vzr

    Jibu

    Sina mashaka na kikosi cha Liver lakini najuwa watakutana na changamoto nyingi lakini bado wananafasi kubwa ya kutetea ubingwa

    Jibu

    Kikosi chake kipo poa hata asipo badilisha#Meridianbettz

    Jibu

    Hatutaki maneno yake,tunasubiri vitendo!!!!

    Jibu

    klopp bado hanakiamini kikosi chake kama bado kipo vizuri

    Jibu

    katika makocha wa sasa ni klopp pekee unayeweza kumpa aston villa na bado akaleta ushindani mkubwa

    Jibu

    Kloop ana kikosi bora sana ila inabid awe na kikosi kipana zaid sana kwakuwa kama
    Akitumia kikos kimoja wachezaji watachoka

    Jibu

    Klopp kikosi chake kikoimala

    Jibu

    Kolopp ni kocha mzuri sana pia kikos chake kipo vizuri sana

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Liverpool bado wapo imara na kikosi chao kile kile na bado wanafanya vizuri kwenye soka

    Jibu

    Safi

    Jibu

    klopp yupo vzr sana#meridianbettz

    Jibu

    Liver bado iko gud.

    Jibu

    Liverpool bdo ipo vzuri

    Jibu

    asante meridianbet kwa habar moto moto

    Jibu

    Nakubali

    Jibu

    Kloop ana Kikosi kilicho bora na inabidi a badili Kikosi kwakua Kikosi alichonacho kitachoka kwa msimu ujao

    Jibu

    Klopp ni kocha mzuri sana

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Klopp namwamini sana

    Jibu

    Klopp ni kocha mzuri sana na anauwezo mkubwa sana

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Super manager.

    Jibu

    Klopp ni kocha mzuri

    Jibu

    Me naon Liverpool inafany usajir wa akili

    Jibu

    Klopp aache kufanya mambo kwa mazoea nyakati ubadilika

    Jibu

    Kikosi cha klopp kimejipanga ipasavyo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.