Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania na aliyekuwa mchezaji wa Aston Villa – Mbwana Samatta, sasa ni rasmi amekamilisha usajili wa kuichezea Fenerbahce ya Uturuki msimu huu.
Samatta alisajiliwa na Aston Villa mwezi Januari akitokea Genk – Ubelgiji. Akiwa Aston Villa amecheza michezo 16 na kuzifumania nyavu mara 2 pekee. Alitua Villa kwa ada ya pauni milioni 10 na alisaini mkataba wa miaka 4 na nusu.
Baada ya kutokuwa na mwanzo mzuri kwenye EPL akiwa na Villa, sasa amesajiliwa Fenerbahce na anakwenda kukipiga katika ligi ya Uturuki. Kwa sasa tayari Villa wameshasajili washambuliaji wawili akiwemo Ollie Watkins na Bertrand Traore.
“Ninajua Fenerbahce ni klabu kubwa. Ninafurahi kuwa kwenye familia hii, itakuwa ni changamoto mpya na kubwa kwangu.
“Fenerbahce inamashabiki wengi na wanahitaji ushindi kila mara. Na mimi ninataka kushinda, nimekuja hapa kwa sababu hiyo. Nimefurahi sana na ninaimani tutashinda makombe mengi.” amesema Mbwana Samatta.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


Leonard
Sio mbaya endelea kupambana
aisha
Ni hatua nzuri ya mbwana samata kuchezea timu ya fenerbahce kila la kher
Venerose
Endelea kupambana bwana mkumbwa
Adelta
Endelea hadi kieleweke
magdalena
kila la kheri samatta kaoneshe maajabu zaidi ata waliokudharau wakuheshimu mwisho wa siku
Rose kapinga
Kazi nzuri pongezi kwako endelea kupeperusha bendera ya,watanzania!!
Mwajumah
Hongera sana samatta kazi nzuri unayofanya ndio inakufikisha ulipo
Ernest
Lets go our Captain, Sam Magoli, Ulipo tupo, Fenerbahce new deal in Tanzania
Tatu
Kila la khery huko uwendako endelea kukiwasha mashabiki tupo nyuma yako
Fatuma kasomo
Safi sana
Sauda
Fenerbahce wamelamba dume
Lydia Emmanuel Magoti
Safii Sana kila La Kheri Sam kwenye makazi yako utayo salia kipige kokote kambi
Dorophina
Samatta amepata dili nono kapambane kijana upeperushe bendera ya Tanzania
Issa
Samata inabid apambane huko arud kwenye hadh yake
Elika
Kila la kheri kaka huko aendako naona hadhi yako inazidi kupanda
Shan
Pongezi kwake zidi juhudi na maharif uzid songa mbele zaid!!
Hopemwaikuka
All in all kapambane tu
Rehema
Asante kwa taarifa
Samiah
Kilalakheri jembe
Khadija
Kila la kheri
Christa
Atafika tu alipokusudia. Hatua kwa hatua
Gabriel
hatua nzuri ya mbwana samata kuchezea timu ya fenerbahce Kila la kheri
Caroline
Sio mbaya Fenerbahce ni timu kubwa.keep it up
Nasra
Safi sana
Zeiyana
Samatta hanazidi kuipeperusha bendela ya Tanzania kila la kheri ulipo nasisi tupo
Frank P
Asipoongeza jitihada ndio mwisho wake wa kuruka ruka huo
Ester jackson
Hongera sana katika timu hiyo ninaimani utapata nafasi nyingi kama utajitema vema mana huko hakuna ubaguzi kwa sababu timu imetawaliwa na wachezaji black
Tumaini kasalile
Tunakunakutakia maisha mema
Fatina mfingi
Mungu akuongoze ukafanye makubwa samatta
Sabrina
Yote sawa piga kazi jembe
Neema
Si sawa tu hata huko alipoenda kikubwa kuongeza juhudii tu
Zahara omary
Daah ila kila hatua dua kila la kheri samatha
Flomena
Good news
Fatina mfingi
Mungu akuongoze ukafanye makubwa samatta
felister
safi samata sisi tunakuombea uzidi kufanya mazuri
Saupha mohamed
Jambbo la kheri
Amiri Kayera
Atafunga sana hapo
Latifa juma mohamed
Deal done , Safi Sana samatta endeleza mapambano.
David Pere
Kila la kheri kaka huko aendako naona hadhi yako inazidi kupanda
Tahiya
Ulipo tupo
Povel
Samatta kila la kheri