Kiungo wa Man United na timu ya Taifa ya Ufaransa – Paul Pogba, bado anandoto ya kuitumikia Real Madrid akiwa kama mchezaji.
Pogba amekuwa akihusishwa sana na Real Madrid haswa baada ya Zinedine Zidane kutamka hadharani hamu yake ya kumuona Paul akitumikia kikosi anachokifundisha.
Maisha yake ya soka yalianzia Man United ambapo alipata umaarufu akiwa bado ni kijana mdogo na baadaye aliuzwa na kujiunga na Juventus.
Akiwa Juve alifanya mambo mengi mazuri akitengeneza safu nzuri ya kiungo na Andre Pirlo ambaye kwa sasa ni kocha wa timu hiyo.
2016 Pogba alisajiliwa tena Man United akiwa katika kiwango cha juu sana. Maisha yake ndani ya United yamekuwa ni ya kupanda na kushuka, msimu baada ya msimu, kiwango chake hakitabiriki na wengi wanahisi bado hajaonesha uwezo ule aliotoka nao Juventus.
Akiwa amebakiwa na mwaka 1 kwenye mkataba wake, pengine wengi tulidhani angesajiliwa na timu kubwa katika dirisha hili la usajili ambapo bado hajaongezwa mkataba mpya na Man United, hali haikuwa hivyo na mpaka sasa ni mchezaji halali wa Man United.
Akizungumza na waandishi wa habari akiwa Ufaransa, Pogba amesema “kila mchezaji angependa kucheza Real Madrid. Ni ndoto yangu, sasa kwanini isitokee siku moja?
“Nipo Manchester na ninaipenda klabu yangu. Ninaichezea Manchester na ninafurahi, ninataka kufanya kila ninaloweza kuirudisha klabu mahali inapotakiwa kuwa. Nitajitoa kwa kila niliwezalo kama ilivyo kwa wachezaji wengine.”
Je, ndoto ya Pogba itatimia? Kuna mengi ya kuendelea kufurahia katika ulimwengu wa soka na hili ni moja wapo.
Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!


Samira
Pogba anawatishia tu man utd wamuongezee mshahara mnono
Angelina
Kambi popote kikubwa maslahi
Magdalena
Pogba anataka kuwatia jambajamba united
Caroline
Pogba mtu mbad
lombo
anaota
Fatuma kasomo
Safi sana
Neema
Inapendeza sana
Issa
Pogba kuenda madrid imekua stor alikua kwenye rada zao lakin sasa hawana uhitaj nae perez anaona hana umuhim wa kupoteza pesa
Povel
Haend tu naona maisha ya United wamefika tamati kwake
Hopemwaikuka
Ukitaka nenda tu kaka
David Pere
Pogba kuenda madrid imekua stor alikua kwenye rada zao lakin sasa hawana uhitaj nae perez anaona hana umuhim wa kupoteza pesa
Mwanahamisi
Safi sana
Adelta
Kikubwa maslai kambi popote
Ernest
Uwezekano upo mkubwa sana kwa Pogba kutua Madrid
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri zitatimia tuu Pogba kilakitu kinakwenda namipango
Venerose
Ana mawazo manzur
Janeflora malisa
🔥
Rehema
Good news
Mariam mtandama
Safi
Sadick
Ni namna ya kujipigia debe ili asajiriwe na wakala wake mpende fedha anafurahia hilo kutokea. Nadhani angeweka akili yake Man U bila kuonyesha hisia zake kwamba angependa kucheza Real Madrid#meridianbettz
Tatu
Pogba akitua Real Madrid itakuwa vizuri naona Man u awana jipya
Sabrina
Itakua poa sana akitua madrid
felister
safi tu
aisha
Pogba nae akae atulie afanye maajabu asiwe mtu mwenye mawenge mara huku mara kule
Nasra
Safi tu
Amiri Kayera
Paul pogba anamsim mzur pale United pengne akiondok atuludsh makali
Zeiyana
Pogba yupo vizuri sana hakuna clabu ambayo hitakataa kumsajiri yeye tu apiganie hatimize ndoto zake
Salma ngende
Vizuri
latifa juma mohamed
Safi sana
Saupha mohamed
Good news
Sauda
Afanye kweli atimize ndoto
Gabriel
maisha ya United wamefika tamati kwake
Fatina mfigi
Safii
Mwajumah
Safi sana
Rose kapinga
Huenda ikawa kwel