Baada ya kugawana pointi kwenye mchezo wa EPL wikiendi iliyopita, Liverpool na Man United walikutana tena kwenye FA Cup jumapili hii.
Vikosi vya timu zote vilibadilika katika mchezo wa mzunguko wa 4 wa FA Cup ambapo ni kombe lenye heshima kubwa kwenye historia ya soka la Uingereza.
Liverpool ilimkosa nahodha wake Jordan Henderson huku Sadio Mane akianzia benchi. United walimpumzisha Bruno Fernandes huku Dean Henderson akichukua mikoba ya De Gea kulinda goli.
Man United vs Liverpool ni mchezo wenye upinzani mkali kwa miaka mingi. Licha ya Salah kuanza kutikisa nyavu za United dakika ya 18, Greenwood alisawazisha na Rashford akaongeza la pili. Muda mfupi baadae, Salah alisawazisha kabla ya Fernandes kuwapatia ushindi United kwa mpira wa faulo dakika ya 78.

Kipigo cha Liverpool kutoka kwa United kinaendeleza takwimu mbaya za Liverpool dhidi ya United katika uwanja wa Old Trafford, Liverpool wameshinda mchezo 1 kati ya 15 waliyocheza katika uwanja huo.
Kwa ujumla, Liverpool anakamilisha michezo 4 bila kupata ushindi katika mashindano yote. Msimu uliopita, Liverpool alitoka katika mzunguko wa 5 wa FA Cup lakini msimu huu, safari yao imeishia mzunguko wa 4.
United watachuana na West Ham United katika mchezo wa mzunguko wa 5 mwezi Februari, 2021.
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!



warda
Fernandes alinikosha sana
Adelta
Good
Venerose
Jambo jema
Rahmal
Safi sana
Sania
Safi sana
Magdalena
United mlifanya kitu kizuri sana
Sarah
Good
Shakila mrope
Safi san inapendeza
Ernest Kimeru
Fernandes anaendela kujenga ufalme wake ndani ya Man U
Dorophina
Fernandes alijua kutufurahisha mashabiki wa man u
Hopemwaikuka
Nakubalii
Lydia Emmanuel Magoti
Fernandes mtu mbaya akoseagi
Angelina
Goodnews
Saupha mohamed
Good
Issa
United inepata