Nyota wa PSG, Neymar amesema suala la mkataba wake mpya na PSG sio ishu na anahisi kuendelea kuwa na furaha klabuni hapo kuliko wakati mwimgine wowote. Neymar amezungumza hayo baada ya PSG kufuzu hatua kwenda nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.
Nyota huyu, ambaye aliwasili PSG akitokea Barcelona kwa €222m mwaka 2017, mkataba wake wa sasa unafika mwisho mwakanni 2022. Pande zote zilitajwa kuwa kwenye majadiliano ya mkataba mpya, mpaka pale Neymar aliporipotiwa kusitisha mazungumzo ya mkataba mpya.
Staa huyu alikuwa anahusishwa na kurejea La Liga, lakini PSG wao wamesisitiza kuwa Neymar hatakuwa sokoni, hata kwa pesa nyingi hawako tayari kumuuza kwa sasa.
Hata hivyo, alipoulizwa juu ya hali yake ya mkataba mpya amebainisha hilo sio tatizo kwa sasa. Akizungumza na ESPN Brazil amenukuliwa akisema;
“Kusaini mkataba mpya, sio tatizo kwa sasa. Kimsingi nahisi kuwa huru na kuwa nyumbani hapa PSG. Nahisi kuwa na furaha kuliko wakati wowote”
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Adelta
Neymar kwa sasa anaifurahiya timu yake kutokana na matokeo mazuri wanayoyapata , hivyo swala ya yeye kutaka kuhama hajalipa kipao mbele.
Venerose
Neymar uko makini
Sarah
Neymar yuko vizuri
warda
Huyu dogo yupo mguu mmoja mnje mmoja ndani