Taarifa zinasema kinda wa Arsenal Folarin Balogun yupo karibu kusaini mkataba mpya, hii ni kwa mujibu wa meneja Mikel Arteta.
Nyota huyu wa kikosi cha vijana cha Uingereza, mwenye miaka 19 alionekana kuwa kwenye maandalizi ya kuondoka kikosini hapo mwisho wa msimu kama mchezahi huru baada ya kushindwa kupenya kwenye kikosi kikubwa.
Hata hivyo, mazungumzo juu ya mkataba mpya yanonekana kuleta matumaini mabya kwa staa huyo huku Arteta akiamini kuwa staa huyo ataendelea kuwepo Arsenal kwa mda mrefu zaidi.
Arterta amenukuliwa akizungumza Jumatano, Arterta alinukuliwa akisema;
“Tutaenda kuliweka hili rasmi pale litakapokuwa rasmi na kila kitu kitakapokuwa tayari kimekamilika. Nimekuwa nikiamini wakati wote kuwa atasalia klabuni hapa. Tunahitaji aendelee kuwepo. Tupo karibu sana.”
Balogun amefunga magoli 55 kwenye mechi 77 za ligi ya vijana akiwa na Arsenal, na pia alicheka na nyavu kwenye kikosi cha watu wazima cha Arsenal kwenye mechi ya Europa dhidi ya Molde na Dundalk.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.
Adelta
Balogun kila la kheri uko uendapo
Venerose
Bidii katika kazi ndio inayo itajika
Sarah
Lila la kheri
warda
Safi sana