Kocha wa Chelsea Thomas Tuchel aeleza furaha yake kusaidia timu yake kuingia nusu fainali ya UEFA kwa mara nyingine toka 2014. Thomas asema kwamba ni mafanikio makubwa sana kwa Chelsea na wanataka kufika fainali kabisa na watafika.
Chelsea walifanikia kutinga nusu fainali ya kombe hilo la UEFA baada ushindi wa jumla wa 2-1, licha ya kupoteza goli moja kwa sifuri dhidi ya Porto hapo jana wakiwa nyumbani.
Kocha wa Chelsea asema anatamani sana kukutana na timu ya Real Madrid kuliko Liverpool. Tuchel alisema hiyo ni kwa sababu anatamani kupata changamoto kutoka ligi nyingine na hiyo ndiyo maana halisi ya michuano ya ulaya.
Real Madrid ana nafasi kubwa ya kushinda mechi hiyo ikiwa na historia nzuri sana ya kuchukua kombe hilo la UEFA kwa mara nyingi zaidi.
Timu nyingine iliyofanikiwa kutinga nusu fainali ni PSG ambao wametoa mabingwa watetezi Bayern Munich baada ya magoli ya ugenini licha ya kupokea kipigo cha 1-0 jana usiku.
PSG atasubiri Mshindi kati ya Dortmund na Man city ili akutane nae nusu fainali. Kwa hakika UEFA ya mwaka huu inafurahisha sana. Je, ndoto ya Tuchel itatimia? atakutana na Madrid au Liverpool? Ataweza Kunyanyua kombe la UEFA tena?
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.
Adelta
Inawezekana kwamba anatamani kukutana Real Madrid katika hatua nyingine ya mtoano na si Liverpool kwa sababu pengine inatoka nchi nyingine tofauti na Liverpool ambao wanacheza ligi moja kwani wanafahamiana vizuri
Venerose
Chelsea kufika fainal mtafika ila kazeni buti
warda
Tuchel nae anasifa sana