Beki wa Simba Joash Onyango amesema ndoto yao kubwa ni kuhakikisha wanaleta nyumbani taji la Caf Champions League.
Miamba hao wa msimbazi wamefurahia muendelezo mzuri kwenye kampeni hii wakiwa tayari wamekata tiketi ya robo fainali kutoka kwenye kundi gumu sana Kundi A ambalo lilikuwa na timu kama Al Ahly ya Misri, AS Vita ya DRC na Al Merrikh ya Sudan.
Simba wamejongea kwenye robo fainali wakiwa ndiyo viongozi wa kundi lao kwa jumla ya alama 13 wakati Al Ahly wakiwa nafasi ya pili kufuzu hatua ya nane bora.
Simba wakiwa wanasubiri droo ambayo imepangwa kufanyika April 30 mlinzi wa Kenya ambaye alijiunga na Simba akitokea Gor Mahia ya FKF Premier League ameeleza lengo lao la kushinda taji la Champions League.
“Ni ndoto ya kila mchezaji kuapata mafanikio na hiyo ndiyo sababu wachezaji wa Simba wamekuwa wakipambana tangu tulipoweka lengo la kushinda taji la Caf na kulileta nyumbani, tunaamini itakuwa hivyo,” Onyango alisema akinukuliwa na Nation Sport.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Venerose
Tunawatakia kika la kheri
Adelta
Tunazidi kuwaombea ili ndoto yenu itimiye
Sarah
Kila lakheri kwao
warda
Nakubali sana maneno yake