Mchezaji Pau Torres anayekipiga katikaklabu ya Villareal amekuwa akifanya vyema sana katika majukumu yake ya ulinzi na kocha mkuu Unai Emery anaonekana kumtumia sana.
Kutokana na ubora wake, Pau amekuwa akihusishwa na kuhitajika na vilabu mbalimbali ikiwemo, Real Madrid, Barcelona na Manchester United. Torres amewekewa thamani ya Euro millioni 56 na Villareal wanaamini klabu kubwa yoyote duniani inaweza kulipa dau hilo.
Muhispania huyo amekuwa na wakati mzuri sana pale Villareal na amejipatia umaarufu mkubwa akiwa na timu ya taifa ya Spain. Ukuta wa ulinzi wa Man United umekuwa ukionekan kusuasua na mtu kama Pau Torres anaweza kuwa ongezo sahihi kabisa kwenye sehemu hiyo ya ulinzi.
Je, wapo tayari kutoa kiwango hicho cha fedha kwa ajili ya kuchukua saini ya nyota huyo? Ukizingatia matatizo mbalimbali ya Korona?
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Adelta
Pau Torres anastahili
Venerose
Kweli kabisa Pau yupo vinzur
Sarah
Pau yupo vizuri
warda
Duuu mipesa yote hiyo