Msemaji wa Simba SC inayoshiriki katika ligi ya Tanzania bara, VPL, Haji Manara ameeleza huzuni yake kwa waandishi wa habari ambao wanaendelea kuizonga Simba licha ya mafanikio makubwa yanayopatikana kwa timu hiyo.
Akizungumza na waandishi bara kuelekea mchezo wa tarehe 3 dhidi ya watani wao wa Jadi, Kariakoo Derby, Manara amedai kuwa kuna baadhi ya waandishi wa habari ambao wanaendesha mbio za kuisema Simba.
Katika mazungumzo hayo, Manara amewataka waandishi hao kujaribu kuandika habari za ukweli ambazo zitaendeleza mpira wa Tanzania na sio kuandika uzushi ili kudhoofisha upande mmoja.
Haji ameeleza kuwa kuna ulazimu wa kutoa taarifa za kweli ili kutenda haki kwa watu wanaohitaji haki husika na si vinginevyo. Haji ameeleza pia kuwa Simba imejiandaa vizuri kuelekea mchezo huo na wanatamani TFF walete kombe kabisa siku ile!
IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!

