Pambano la Tyson Fury la kutetea taji lake la ndondi za uzani wa juu dhidi ya Deontay Wilder, lililopangwa kufanyika Julai 24, limeahirishwa rasmi.
Baada ya majibu ya vipimo vya coronavirus vya Tyson Fury, pambano hilo la tatu kwa mabondia hawa kukutana ulingoni limepangwa tena hapo Oktoba 9.
Wiki iliyopita iliripotiwa kwamba Fury alikuwa ameambukizwa Covid-19 na hiyo ikalazimisha kuchelewa kwa mipango ya pambano lake kulinda taji la WBC dhidi ya Wilder.

Alinukuliwa akisema: “Sitaki chochote zaidi ya kumvunja ‘Big Dosser’ hapo Julai 24, lakini nadhani kipigo kitasubiri. Usikosee, nitarudi nikiwa bora kuliko awali. Tutapambana Oktoba 9 na nitamgonga kwa KO.”
Meneja wa Wilder Shelly Finkel ameongeza: “Hivi ndivyo tulivyokubaliana kwenye usuluhishi. Bado yupo tayari kutetea taji lake la ulimwengu mnamo Oktoba 9.”
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


