Klabu 5 Zinazowinda Saini ya Pierre-Emerick Aubameyang

Pierre-Emerick Aubameyang anaripotiwa kuwa windoni kwenye rada za vilabu vitano huku kukiwa na uvumi kuhusu hatma yake na Arsenal.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 ameshindwa kuonesha kiwango chake cha kawaida kwa miezi 12  iliyopita.

Mkataba wa sasa wa Pierre na Washika Bunduki unadumu hadi 2023, hii ni baada ya kuongeza mkataba wake msimu wa joto uliopita, lakini anaendelea kuhusishwa na kuondoka akionekana kushindwa kufanya vyema mbele ya nyavu.

Kwa mujibu wa Fichajes, Real Madrid, Barcelona, Atletico Madrid, Inter Milan na AC Milan zote ziko tayari kupambania saini ya Aubameyang mwaka 2022.

Aubameyang Aomba Radhi kwa Kupata Sare na Benfica.
Aubameyang

Ripoti hiyo inadai kwamba siku za staa huyu na Arsenal zinahesabika, na huenda akapewa tiketi ya kuondoka Januari mwakani huku Arsenal ikilenga kupokea ada kubwa kwenye biashara ya mshambuliaji huyo.

Aubameyang ana jumla ya mabao 92 katika michezo 162 akiwa na The Gunners kwa michuano yote lakini kwa sasa ameshindwa kuzitendea haki nyavu katika mechi tano mfululizo za Ligi Kuu ya Uingereza.


MUDA WA KUJIACHIA NA CARNAVAL JACKPOT

Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.