Baada ya ushindi wa 3-0 wa Borussia Dortmund dhidi ya Greuther Furth Jumatano, Erling Haaland alionekana akipunga ncha zote nne za Signal Iduna Park katika kile kilichotafsiriwa kama ishara ya kuaga baada ya kufunga bao mbili na kuipa timu yake pointi zote tatu.
Hata hivyo, mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo, Michael Zorc, aliwahakikishia mashabiki baada ya mechi ya mwisho ya Dortmund mnamo 2021 kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway atasalia kwenye dirisha la usajili la Januari.
“Nilimuuliza nini kilikuwa nyuma ya ishara hiyo na hakujibu chochote,” Zorc aliambia Sky Sports Germany.
“Bila shaka atasalia. Bila shaka tungependa abaki Dortmund majira ya joto. Hatufai kumwachia, si kwa sababu za kifedha pia.
“Lakini pia tunajua kwamba chini ya hali fulani ana nafasi ya kubadilisha [vilabu] na bila shaka tutakuwa na mazungumzo naye katika wiki zijazo.
“Tuna mkataba wa muda mrefu naye, hivyo anatakiwa kuchukua hatua kwanza na sio sisi. Kila kitu kitakuwa sawa kwa Dortmund ikiwa itaendelea kuwa hivyo.”
Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.


