Eddie Nketiah anaripotiwa kuwa bado yupo tayari kuondoka Arsenal wakati wa dirisha la usajili la Januari.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 alifunga hat-trick mapema wiki hii huku The Gunners wakiandikisha ushindi wa 5-1 dhidi ya Sunderland katika mechi ya robo fainali ya Kombe la EFL.
Hata hivyo, mhitimu huyo wa akademi amecheza kwa dakika 38 pekee za soka la Premier League msimu huu, ikiwa ni sababu yake ya msingi ya kukataa mkataba mpya klabuni hapo.

Licha ya Mikel Arteta kusema mara kwa mara kwamba anataka huduma za fowadi huyo, gazeti la Daily Mail linasema kwamba kwenye soko la Januari mambo yanaweza kubadilika.
Pamoja na kuweza kusaini mkataba wa awali wa kandarasi na klabu ya kigeni, Nketiah anavutiwa na timu nyingine za ligi kuu ya Uingereza, zikiwemo West Ham United, Crystal Palace na Brighton & Hove Albion.
Uamuzi wa kumuuza Nketiah yanategemea ikiwa Arteta atasuluhisha hali yake inayoendelea na Pierre-Emerick Aubameyang, ambaye anaweza kuruhusiwa kuondoka kwenye Uwanja wa Emirates kutokana na utovu wake wa nidhamu wa hivi punde.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


