Cancelo Arefusha Kandarasi Yake na Man City

Joao Cancelo ameongeza mkataba wa miaka miwili utakaomweka Etihad hadi 2027, Manchester City walitangaza siku ya Jumanne.

Cancelo Arefusha Kandarasi Yake na Man City

Beki huyo wa pembeni wa kimataifa wa Ureno amejidhihirisha kuwa mchezaji muhimu wa kikosi cha Pep Guardiola tangu awasili kutoka Juventus mwaka 2019, akicheza michezo 106 na kushinda mataji matatu makubwa.

Vilevile  anaweza kucheza beki ya kulia, kushoto au katikati, anafanya kazi kwa kiwango sawa cha juu.

“Manchester City ni klabu nzuri sana, kwa hivyo nina furaha kubwa kusaini mkataba huu mpya,” alisema mchezaji huyo wa miaka 27.

“Wachezaji wa City wana kila kitu wanachohitaji kufikia uwezo wao kamili, na vifaa vya kushangaza, wachezaji wa kiwango cha kimataifa na meneja wa ajabu ambaye hutusukuma kila siku.

Cancelo Arefusha Kandarasi Yake na Man City

Mkurugenzi wa soka wa City, Txiki Begiristain, alisema: “Joao ni mchezaji wa hali ya juu. Anapenda sana mpira wa miguu na anajituma kila siku kwa nia ya kuwa bora zaidi.”


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.