Timu ya Taifa ya Tanzania ya mchezo wa Pooltable imeendelea kupeperusha vyema bendera ya nchi baada ya kupata ushindi katika michezo yake miwili iliyocheza jana, Februari 6, 2025.
Katika mchezo wa kwanza, Tanzania iliifunga Zimbabwe kwa fremu 14-11 kabla ya kuendeleza moto huo kwa kuwachapa wenyeji Afrika Kusini kwa ushindi mwembamba wa fremu 13-12 katika pambano lililokuwa na ushindani mkubwa hadi fremu ya mwisho.
Ushindi dhidi ya Afrika Kusini umeonekana kama kisasi kilicholipwa, kufuatia kumbukumbu ya fainali za mwaka 2023 ambapo Tanzania ilipoteza kwa fremu 11-13 dhidi ya wapinzani hao.


