Kocha wa klabu ya Liverpool Jurgen Klopp anatarajia kumuona Erling Haaland majira ya kiangazi kwenye klabu ya Manchester City naa kusema kuwa ataleta level mpya ya ushindani kwenye ligi hiyo.
City wanjaianda kulipa ada ya kuvunja mkataba kwa klabu ya Borussia Dortmund kiasi cha €75 million ili kuweza kumleta nyota huyo hatari kwa sasa barani ulaya.

Klopp ambaye amesaini mkataba mpya ambao utamuweka kwenye klabu ya Liverpool hadi mwaka 2026 na amesema kuwa hajavunjika kwamba washindani wake kuwa na nguvu zaidi, lakini amekubali kwamba Haaland ataleta nafasi mpya kwenye ligi kuu ya Uingereza.
“Nimesaini mkataba mpya nikijua kwamba City hawataacha kukiboresha kikosi chao. City hawawezi kutuamulia furaha yetu, ni kuhusu sisi,” Jurgen Klopp alisema
“Kama Erling Haaland akienda city, haitatu nyong’onyesha uwezo wetu. Haiwezi kabisa.
“Najua kwa kipindi hiki watu wengi watazungumzia kuhusu pesa, lakini mimi wacha niseme usajiri huu utaleta hali mpya, wacha mimi niseme hivi.”
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.