Arsenal wanaendelea kumfuatilia kwa karibu mshambuliaji wa Bayer Leverkusen, Christian Kofane, kabla ya uwezekano wa uhamisho majira ya joto.

Arsenal wako tayari kutumia fedha nyingi kumsajili mshambuliaji huyo kijana wa Leverkusen, kwa mujibu wa mwandishi wa Sky Germany, Florian Plettenberg.
Kofane alijiunga na klabu hiyo ya Ujerumani kutoka Albacete majira ya joto yaliyopita, na licha ya kutopata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza, kijana huyo wa miaka 19 ameonyesha kiwango kizuri kila anapopewa nafasi.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon, ambaye alifunga mabao mawili kwenye Africa Cup of Nations, ameanza mechi tisa za ligi msimu huu.
Licha ya kucheza muda mdogo, ameweza kufunga mabao matano na kutoa pasi tatu za mabao katika Bundesliga msimu huu.

Kijana huyo alicheza dakika zote 90 katika mechi zote mbili za UEFA Champions League dhidi ya Arsenal, na ingawa hakufanikiwa kuisaidia Leverkusen kusonga mbele, aliwavutia viongozi wa klabu hiyo ya Uingereza.
Arsenal sio timu pekee inayomfuatilia, kwani vilabu kadhaa vya England pamoja na Real Madrid pia vinaonyesha nia kwa mujibu wa Plettenberg.
“Arsenal wanamfuatilia Christian Kofane. Mshambuliaji huyo mwenye miaka 19 alivutia katika robo fainali ya Champions League,” aliandika Plettenberg kwenye X.
“Vilabu vingine vikubwa vya Uingereza pia vinamuhitaji, na Real Madrid pia wanamfuatilia. Bayer Leverkusen wanataka euro milioni 60 hadi 70 kwa uhamisho wa majira ya joto. Ni dili kubwa lililoandaliwa na Simon Rolfes na Falkenberg, ambao wako kwenye mawasiliano mazuri na wakala Eric Depolo.”
Arsenal wanatarajiwa kuongeza nguvu kwenye safu yao ya ushambuliaji majira haya licha ya kutumia pesa nyingi msimu uliopita.
Timu ya Mikel Arteta ilimsajili Viktor Gyökeres kutoka Sporting CP majira ya joto yaliyopita, lakini Mswizi huyo amekuwa na mwanzo wa wastani katika dimba la Emirates.


