Giovan Van Bronckhorst anatajwa kuwa ndie atakae wanaoa Mabingwa watetezi katika ligi kuu ya nchini Scotland Rangers, muda wowote kuanzia sasa watamtangaza gwiji wa zamani vilabu mbalimbali barani ulaya kuwa kocha wao mpya
Timu hiyo yenye maskani yake kwenye mji wa Glasgow nchini humo ipo mawindoni kumtafuta kocha mpya tangu kocha wake Steven Gerrard atimkie Aston villa
Bronckhorst ambaye pia aliwahi kuwa mchezaji wa Rangers katika miaka 1998 hadi mwaka 2001 akishuhudiwa akishinda mataji matano makubwa
Siku ya jana alikuwa kwenye kikao cha mwisho na wamiliki wa timu hiyo nchini Uingereza huku utangazwaji wake wa ukocha mkuu ukitarajiwa kutangazwa ndani ya masaa 24 yajayo
Giovan Van Bronckhorst ,46,msimu wa mwaka 2017 alishinda taji la ligi kuu na vikombe viwili vya ligi nchini Uholanzi akiwa na Feyenoord kabla ya kutimkia ligi ya China ambapo hivi sasa alikuwa hana kazi baada ya kuibuka kwa virusi vya uviko nchini humo.
Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.