Mchakato wa Liverpool kumnasa Saul Niguez unatajwa kuwa upo kwenye hatua nzuri baada ya Atletico Madrid kumleta Rodrigo De Paul kama mbadala wa kiungo huyo.
Liverpool wanasemekana kuongoza vilabu vingi vinavyoiwinda saini ya mchezaji huyo wa miaka 26, ambaye alipambana kuanza mara kwa mara chini ya Diego Simeone kwenye kampeni ya 2020-21.

Saul bado ana miaka mingine mitano ya kuendelea kuweko klabuni hapo kwa mujibu wa kandarasi iliyosainiwa 2017, lakini mchezaji huyo wa Atletico anaaminika kuwa mbioni kuondoka msimu huu wa joto.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


