Tudor Atoa Ujumbe wa Moto Kabla ya Mchezo Dhidi ya Liverpool FC

Kocha wa Tottenham Hotspur, Igor Tudor, ametoa ujumbe wa wazi kwa wachezaji wake kabla ya mchezo wa ligi dhidi ya Liverpool FC utakaochezwa Jumapili mchana katika Anfield. Tudor, ambaye amepoteza michezo yote minne tangu aingie kama kocha wa muda badala ya Thomas Frank, anajitahidi kuiondoa timu yake katika nafasi hatarishi ya kushuka daraja.

Tudor Atoa Ujumbe wa Moto Kabla ya Mchezo Dhidi ya Liverpool FCTottenham sasa wako na pointi moja tu juu ya West Ham United waliopo nafasi ya 18 na Nottingham Forest waliopo nafasi ya 17, na wanapaswa kupata pointi dhidi ya Liverpool na Forest wiki ijayo ili kuendelea kuwa katika ligi ya juu. Tudor alimwambia kikosi chake kuwa ni lazima wasimame wakiamini uwezo wao na kuanza kupigania kila hatua. Alisema

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Hali ni ngumu. Sio tu kwa mchezo wa mwisho lakini kwa kipindi chote. Sio rahisi, ni changamoto kubwa kubadilisha mambo. Kama katika maisha yote, unaweza kuchagua jinsi ya kuona hali hii. Unaweza kulia au kupigana. Unaweza kuwa mwathirika, au unaweza kubadilisha jambo. Ujumbe huu ndilo nimeuwaeleza wachezaji. Chupa inaweza kuwa nusu tupu au nusu jaza. Wale watakaosimama na ujasiri wa kubadilisha mambo hawa watakuwa watu na wachezaji bora baadae. Ni juu yetu sote, si kuhusu mabishano yasiyo na maana.”

Tudor Atoa Ujumbe wa Moto Kabla ya Mchezo Dhidi ya Liverpool FCAidha, Tudor alibainisha hali ya wachezaji kabla ya mchezo, akithibitisha kuwa Joao Palhinha na Cristian Romero hawatacheza, huku Micky van de Ven na Yves Bissouma pia wakiwa nje kwa majeraha, ingawa Conor Gallagher ana dalili za homa lakini huenda atacheza.

Tudor aliongeza kuwa kikosi chake kina changamoto nyingi kuunda kikosi cha mwanzo kutokana na majeraha na kadi nyekundu zilizotokea katika michezo ya awali, lakini anasisitiza lazima wakubali hali hiyo na kujaribu kubadilisha mambo yanayoweza kubadilishwa huku wakiendelea kupigania.

Tudor Atoa Ujumbe wa Moto Kabla ya Mchezo Dhidi ya Liverpool FCRipoti zinaonyesha kuwa Tudor anaweza kufutwa kazi ikiwa atapoteza mchezo wa tano mfululizo, huku majina kama Sean Dyche yakiwa tayari kuchukua nafasi hiyo, jambo litakalofanya Tottenham kuwa na kocha wa nne katika msimu ambao umekuwa mgumu sana.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.