
Virgil van Dijk amesema kwamba Liverpool inaenda kuwa bora na kutawala amevionya vilabu vya Ligi ya Uingereza. Liverpool wapo kileleni mwa ligi ya EPL kwa tofauti ya alama 22 huku zikiwa zimesalia mechi 9 ligi kumalizika.
Siku ya juni 21 Liverpool watakutana na Everton ikiwa ni mchezo wao wa kwanza tangu kurejea kwa ligi ya EPL baada ya kusimama kwa muda kufuatia kutokea kwa virusi vya Korona Liverpool wakialikwa katika dimba la Goodison Park.
“Najua kiasi gani mashabiki wetu wamekuwa wakisubiri hili,” Van Dijk alisema kupitia Daily Mail “Kwa bahati mbaya hawatapata kushuhudia hili kama likitokea, tumeona vilabu vingine katika mataifa meingine wakishinda mataji bila uwepo wa mashabiki uwanjani.
“ Kwangu mimi kushinda taji la Premier League na kulinyanyua juu ingekuwa nikutimiza ndoto. Mwaka jana tulikaribia kulipata kombe hili lakini mwaka huu tupo karibu sana, tuna michezo tisa na tutajitahidi tushinde yote. Hilo ndio lengo letu.

“Kwa ushindi wa michezo miwili tuu, tutakuwa mabingwa wa EPL. Lakini hatutoishia hapo,tunataka kusonga mbele ,tunataka tufanye hivyo na msimu ujao sababu tutaanza msimu vizuri sana baada ya kumaliza msimu huu. Mkurugenzi wetu aliongea nasi vizuri na alisema tucheze vizuri michezo tisa iliyo baki hii itatufanya tuwe na muendelezo mzuri msimu ujao.
“Hatujashinda taji bado. Hatujashinda kitu chochote bado, lakini lengo ni kuuanza msimu unaofuata kwa mtindo ule ule tulio anzanao msimu huu. Tuna weza kuwa ni timu yenye muendelezo, tuna wachezaji wenye uwezo na kupiga hatua katika maendeleo yao. Kushinda ligi itakua uzoefu mkubwa ambayo inaweza kuwapeleka katika hatua bora.
“Tuta jaribu kuzingatia kwenye michezo tisa iliyo salia natumaini tutakuwa na kasi ya kujianda na msimu mpya tukiwa ni mabingwa na tuweze kulitetea taji.
Tangu mwaka 1990 Liverpool hawajaweza kushinda taji la EPL hivyo wakifanikiwa kushinda taji msimu huu itakuwa ni taji lao lao la kwanza ndani ya kipindi cha miaka 30. Pia mashabiki hawatokuepo uwanjani kutokana zuwio lililowekwa na Serikali ya nchi hiyo sababu ya kuwepo kwa Virusi vya Korona.


Aziza mushi
Asanten kwa taarifa meridianbet.
Rehema
Asante kwa taarifa meridianbet
David Pere
Anajidanganya tu nilikuwa na mabeki wenye uwezo kuliko yeye na hajawahi kusema hivyo
Sadick
Natamani kuona Liverpool ikichukua Ubingwa msimu huu. Imefanya bidii nyingi kufikia hatua hii#meridianbettz
Samira
Van Dijk yupo sahihi watajitahidi sana na wasilegeze kamba katika mechi hizo tisa silizobaki waweze kufikia lengo lao la kunyanyua kikombe msimu huu
Evaluziga
Asanteni kwa taarifa nzuri sana
neema hassan
Asante kwa makala#meridianbettz
Genia Sikaluzwe
Ahsant sana meridianbet kwa taarifa
Sylvester
Huu ni msimu wa Liverpool kutawala kwani wachezaji wengi wanaonekana kuchoka sasa na kama leo wanapigwa na Everton hivi #meridianbettz
Antony Luseno
Kwa msimu huu kila mtu kakubali ila msimu ujao wajipange sana
Njiku
Mechi zilizobakia nichache sana hivyo bhasi wakishinda game yao na everton watakuwa pazuri maana watakuwa mbele kwa tofauti ya pwenti 25 dhidi ya wapinzani wake man city,michezo iliyosalia ni michezo 9 ina jumla ya pwenti 27 kama liverpool atashinda game tatu mfululizo itakuwa haina haja atatawazwa na kuwa bingwa wa EPL so ngoja 2one kwanza na everton
Neema hassan
Asante kwa habari#meridianbettz
Issa
Livepool wapo poa sana yupo sahihi
Kenani
Safi kabisa
Shafii
Van Yuko sahihi kwani Liverpool kwa Sasa inawachezaji wazuri na waliokaa pamoja zaidi ya misimu miwili so chemistry yao iko vizuri watasumbua Sana EPL kwa misimu ijayo
Lydia Emmanuel Magoti
Kwamsimu huu kilamtu kakubali ila msimu hujao wajipange kisawa sawa
isha
Uko sahihi liverpool iko powa sana
Devotha
Nataka kuona Liverpool wanachukua ubingwa msimu huu na misimu miwili ijayo
Khadija
Kwa msimu huu Kila mtu kakubali ila wajipange kwa msimu hutakaokuja#meridianbettz
Dorophina
Tnx meridian kwa taarifa za kimichezo
Magdalena
Liverpool lazima ifanye vizuri Sana sababu kocha wao anajua no jinsi gani ya kupangilia wachezaji wake kwa umakini hatumii pupa
felister
mpira dk 90 ngoja tuone hatutaki maneno maneno
Caroline
Inabidi wakaze buti
Omary lukumbi
Van dijk hajakosea huu mwaka wao wamefanya vzr wamesota sana mpk hapa walipo fikia sasa kiukweli wana stahili sifa ila sasa wasijiongopee kwa msimu ujao maana kila timu inaji.imalisha sasa kwa ajili ya msimu ujao bingwa mpk sasa tayar Liverpool kwa mech zilizobak kua bingwa n chache.ila kwa kusema mpk msimu ujao atakua moto hilo asahau vilabu kibao vinafanya usajili wa kina mnoo ili kue na ushindan wa maana msimu huu sawa ila sio msimu ujao
Ester jackson
Liverpool watatamba sana wakichukua ubigwa mana hasaivi hawajachukua lakini wanatamba ila wachukue tu mana wamejitahidi sana kuonyesha ujuzi wao uwanjani
Hamidu
Next msimu utashindana & man utd.. Najua msimu huu ni wenu tusubili msimu ujao timu zitAjipanga je! #meridianbettz
Christopher
Ushindi muhimu kwa mechi zilizosalia hzo
Furahav
Liver msimu huu watachukua tu.
Zeiyana
Ki ukweli wana staili sifa ila sasa wasijiongopee kwani kila timu inajiamalisha kwa ajili ya msimu ujao
Theckla
Van dijk yuko sahihi sana
Elika
Van Yuko sahihi kabisa pia wakubali ama wakatae Liverpool ni mabingwa tuu msimu huu
Povel
Thnks meridian bet kwa information
Neema
Mie naamini wakikaza butii ushindi ni lazima wauchukue tripu hii Liverpool wataongoza
Mwanaidi
Duuh EPL kazi wanayo safari hii
Sabrina
Maoni:liverpool jeshiii
Hope mwaikuka
Axante kwa habar
Frank Patrick
Future Capitain kaongea VVD best of lucky kwa chama langu
Amiri Kayera
Kwa msimu ujao siwaon Liverpool
Leonard
Liverpool ubingwa ni wao
Edgar
kiufupi livepool ubingwa upo mikononi nasio timu ya kumuacha mtu dimbani ni kichapo
Ernest
Kiufupi tuu Liverpool hana mpinzani msimu huu na ni Bingwa tayari
Tahiya
Kwa msimu huu Liverpool nyota imeghara
Hidaya
Liverpool hana mpinzani
Latifa juma mohamed
Taarifa Safi na meridian bet
mwakalosi
liver nao wanaanza kimdomo mdomo kama arsenal
Samiah
Hakuna mpinzani liverpool
Fatuma kasomo
Liverpool hana mpinzani
warda
Acha wachukue tu mana wamelisotea sana#Meridianbettz
Mwanahamisi
Liverpool jeshi la mtu mmoja
Theonestina
Liverpool jeshi kubwa
Salma
Liverpool wanamalizia vizuri ushindi utaenda kwao
Gabriel
Asijiamini sana kwan alama 22 si kitu maana wamebakiza mechi 9 matokeo yanaweza kubadilika kwan hawakumbuki msimu uliopita walivyoanza vizur wakaja kukuta mabadiliko baadae japo anaweza kusema kwakuwa yeye ni beki lakini mpira unamabadiliko Liverpool wasijitanfazie ubingwa mapema kiasi hicho
Amani
Imefanya bidii nyingi kufikia hatua hii#meridianbett
Asia Abdy
Bonge la makala#meridian
nasra
Ushindi kwa Liverpool
Angelina
Tuna imani na liverpol