Bosi Mpya Yanga Aahidi Jambo

BAADA ya kuteuliwa kuwa Ofisa Habari wa klabu ya Yanga, Ally Kamwe ameahidi kufanya kazi kwa ubunifu mkubwa ndani ya klabu hiyo.

Kamwe ambaye alikuwa mchambuzi wa soka alitangazwa jana akichukua nafasi ya aliyekuwa Ofisa Habari wa klabu hiyo ambaye mkataba wake ulimalizika, Hassan Bumbuli.

 

Bosi Mpya Yanga Aahidi Jambo
Afisa Habari wa Young Africans-Ali Kamwe

Akizungumza baada ya kuteuliwa Kamwe alisema kuwa “Namshukuru Mungu kupata nafasi hii ya kuitumikia klabu kubwa kama Young Africansa na nimefurahi sana.

“Ni changamoto mpya kwa upande wangu lakini ninawaahidi mashabiki na wanachama wote wa Yanga kufanya kazi kwa ubunifu na weledi mkubwa katika kuhakikisha mipango ya klabu inafanikiwa.”Afisa Habari wa Young Africans-Ali Kamwe

 

Vijana Wapya Yanga Kazi Kazi
Mkuu wa Idara ya Digitali na Maudhui-Priva Abiud Shayo((Privadinho)

Acha ujumbe