GAMONDI MPAKA 2026 YANGA

Yanga SC imepanga kumuongezea mkataba wa miaka miwili kocha raia wa Argentina Miguel Gamondi utakaomalizika mwaka 2026.

 

Yanga wamefikia hatua hiyo baada ya kuridhishwa na ubora wa Kocha huyo, huku mipango ikiwa ni kuwa na mwalimu ambaye ameshazijua njia za ushindi.

 

Ali Kamwe ameiambia Meridian Sports kuwa, mpango huo umeshakamilika na Gamondi ataongeza mkataba mpya muda mfupi Baada ya kurejea kutoka mapumzikoni.

 

Gamondi mkataba wake ulikua unaisha kabla ya msimu kuanza na uongozi umeona ipo sababu ya kumpa mkataba mpya.

 

“Kila kitu kipo sawa na akirejea kutoka mapumzikoni atamalizia suala hilo,” alisema.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.