Mechi nyingine itakuwa ni pale Uhuru ambapo KMC baada ya kushinda mchezo wake uliopita atamleta nyumbani Ihefu ambaye nae amepata ushindi mechi yake iliyopita.
Mchezo huo utakuwa ni majira ya saa 10:00 mchana huku kila timu ikihitaji pointi 3 muhimu ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya juu kabla mechi hazijaanza kuchanganya hapo baadae.
KMC yupo nafasi ya 6 kwenye msimamo wa ligi akiwa na pointi zake 7 huku kwa upande wa Ihefu wao wanashikilia nafasi ya 8 wakiwa na pointi 6 hivyo tofauti ni pointi moja pekee.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili, vijana kutoka Mbeya waliondoka na ushindi wa bao moja kwa bila. Je leo hii Walipa Ushuru wanaweza lipa kisasi?