Klabu ya Abha FC ya nchini Saudi Arabia imevunja mkataba wa mkopo na winga wa zamani wa Simba SC Luis Miquissone na sasa atarejea kwenye timu yake ya Al Ahly ambayo tayari kwa upande wao wamethibitisha taarifa hizo. Pata Odds kubwa za soka ukiwa na Meridianbet.

Mabingwa hao mara nyingi wa klabu bingwa Afrika sasa huenda wakafungua milango ya maombi kwa timu nyingine kuomba nafasi ya kumsajili Miquissone kwa mkopo wa muda mrefu zaidi.
Inaaminika kuwa Mabingwa mara 28 wa Ligi kuu ya Tanzania Yanga wameonyesha nia ya kumtaka kwa mkopo Miquissone lakini wamezungumza tu na mchezaji na si Al Ahly. Ukiwa na meridianbet unaweza kubashiri mubashara, tembelea maduka ya meridianbet uweze kubashiri.

Lakini kwa mujibu wa Taarifa kutoka moja ya Viongozi wa Simba alisema kuwa kwenye mkataba wao wa kumuuza Miquissone kwenda Al Ahly kuna kipengele kimoja kinawataka endapo watahitaji kumuuza au kumtoa kwa mkopo klabu ya kwanza kupewa nafasi hiyo ni Simba.
Je kabla ya dirisha la usajili kufungwa huenda tukamuaona Luis akaichezea timu yake ya zamani Simba au Yanga? Beti na Meridianbet mechi za ligi zote, odds ni kubwa sana, Usikose hii!!.

