Kocha wa timu ya vijana Simba, Selemani Matola, ameshatua katika ardhi ya Ghana kwenye mashindano ya vijana chini ya miaka 23 yatakayodumu kwa siku nne,
Matola amesema siyo kweli kwamba anafuata wachezaji nchini humo, bali Simba wamepewa mwaliko maalum na yeye ndiye ameruhusiwa kwenda na uongozi kwa ajili ya kuangalia jinsi wenzao wanavyofanya ili kupata timu bora ya vijana,
” Ni kweli naondoka Simba na huu ni mwaliko ambao tumeupata Simba na kwa lengo la kujifunza kupitia kwa wenzetu namna wanavyofanya kujenga timu zao. ”
” Ikitokea nimeona kijana anayefaa basi nitawasilisha hilo kwa uongozi walifanyie kazi lakini siyo kweli kwamba nakwenda kusajili, mwezi ujao nitakwenda tena nchini Comoro kwenye mashindano kama haya, ” alisema Matola.
Nikisharudi ndiyo tunaanza rasmi programu ya maendeleo ya soka la vijana, nafikiri utakuwa muda mzuri tofauti na ilivyo sasa alisema kocha huyo wa zamani wa Lipuli ya Iringa

