Mtibwa Sugar Anaweza Kutoboa Kesho?

Katika mwendelezo wa Ligi kuu ya Tanzania Bara michezo kadhaa kupigwa hapo kesho ambapo klabu ya Mtibwa Sugar watakuwa nyumbani kuwaalika Coastal Union ya Tanga baada ya kutoka kupoteza mechi iliyopita.

 

Mtibwa Sugar Anaweza Kutoboa Kesho?

Mtibwa imepoteza michezo mfululizo kwenye Ligi kwa vichapo vikubwa ambapo hapo kesho wataenda kujiuliza dhidi ya Wagosi wa kaya ambao wao wametoka kutoa sare walipokuwa ugenini.

Coastal Union yupo nafasi ya 11 baada ya kucheza michezo 9, ameshinda michezo mitatu sare sare 3 na kupoteza michezo mitatu huku wakiwa na pointi 12 kwenye ligi hadi sasa, wakati kwa Walima miwa wao wana pointi 15 hadi sasa baada ya kushinda michezo minne, sare tatu na kupoteza mara 4.

Mtibwa Sugar Anaweza Kutoboa Kesho?

Mechi mbili za msimu uliopita timu hizi zilipokutana Mtibwa Sugar alijichuklulia alama nne baada ya mechi ya kwanza kushinda na mechi ya pili kutoshana nguvu kwa kutokufungana.

 

Acha ujumbe