Azam kuivaa Mtibwa kesho

Kikosi cha Azam FC kimeondoka jana alhamis Jijini Dar kuelekea Morogoro kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar.

Mchezo huo utapigwa kesho Novemba 12 mwaka huu kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Akizungumza baada ya kuwasili Morogoro, Kaimu Ofisa Habari wa Azam FC, Hasheem Ibwe alisema: “Kikosi chetu kimewasili mkoani Morogoro salama kwa ajili ya mchezo wetu wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar.

“Tuna jumla ya wachezaji 29 pamoja na benchi la ufundi likiongozwa na Kali Ongala pamoja na Agrey Morris.

“Morali ipo juu kwa wachezaji na leo asubuhi kikosi kimefanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Jamhuri na tupo tayari kwa mchezo wa kesho.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.