Kocha wa klabu ya Yanga Nassredine El Nabi amefungiwa na bodi ya ligi kuu baada ya kutoa maneno makali kwa waamuzi wa akiba katika mchezo namba 38 wa ligi kuu ya NBC.
Kocha Nabi anakumbana na adhabu ya kufungiwa michezo mitatu na faini ya shilingi laki tano baada ya kuthibitika alitoa maneno hayo kwa waamuzi wasaidizi waliokua nje wakati mchezo ukiendelea.
Katika mchezo huo uliopigwa jijini Mbeya huku klabu ya Yanga ikipokea kipigo cha mabao mawili kwa moja na kusitisha rekodi yao ya kutokufungwa katika michezo 49 ya ligi ya NBC,Ndipo kocha huyo alionekana akirushiana maneno na waamuzi wasaidizi waliokua katika katika mchezo huo.
Hii imekua sio mara ya kwa kocha wa Nabi kufungiwa kutokana na kosa la kurushiana maneno na waamuzi katika michezo ambayo klabu yake imekua kwenye wakati mgumu uwanjani. Hivo kocha huyo atakosekana katika michezo mitatu ya klabu ya Yanga.

