Timu ya wanawake ya Simba “Simba queens” Imepangwa katika kundi A ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa Wanawake, pamoja na timu zingine kutoka mataifa mbalimbali Afrika.
Droo hiyo Iliyofanyika hii leo imeweka wazi hatma ya timu hiyo kwa kujikuta wameangukia kundi A wakiwa na timu kama AS Farbat ya Morocco, Green Buffaloes ya Zambia na Determine Girls FC ya Liberia.
Simba Queens walifanikiwa kufuzu mashindano hayo yatakayofanyika Morocco mwaka huu 2022, hii ni baada ya kuibuka washindi wa CECAFA ambapo Timu hiyo ilishinda kwa bao moja dhidi ya She Corperate FC.