Klabu ya Singida Big Stars baada ya kutoa sare ya Mbeya City watakuwa ugenini hapo kesho kuzichapa dhidi ya Dodoma Jiji majira ya 2:15 usiku katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Singida wameanza msimu huu vizuri toka wapande ligi kuu kwani mpaka sasa wapo nafasi ya nne kwenye msimamo wakiwa wamejikusanyia pointi zao 31 baada ya kushinda mechi zao 9 sare nne na kupoteza mara 4.
Wakati wenyeji wao Dodoma bao wanajikongoja kupanda nafasi za juu ambapo wapo nafasi ya 12 baada ya kupoteza mchezo uliopita, huku wakiwa hawana mwendelezo mzuri wa matokeo.

Wameshinda michezo mitano pekee kati ya 17 waliyoshuka dimbani, wakienda sare mara tatu, kupoteza mara tisa na kujivunia alama 18 ambazo bado sio salama mpaka sasa kama wanataka kubakia kwenye Ligi msimu ujao.
Mechi ya kwanza kukutana walitoa suluhu. Je hapo kesho nani kuibuka kidedea na kuondoka na pointi zote 3?

