Yanga na Ihefu Kusaka Pointi 3 Dimba la Mkapa.

Ligi kuu ya NBC kuendelea hii leo kwa michezo miwili ambapo katika Dimba la Mkapa pale Yanga watawaalika Ihefu FC kusaka pointi 3 ambazo walizipoteza mchezo waliokutana mara ya kwanza.

 

Yanga na Ihefu Kusaka Pointi 3 Dimba la Mkapa.

Yanga ilipoteza mechi yake ya kwanza msimu huu kwa Ihefu kwa kuchapwa mabao 2-1 mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika na hawakuamini kilichokuwa kinatokea kwani kipindi hicho timu hiyo ilikuwa inashikilia mkia.

Leo hii wanakutana tena huku vijana wa Nabi wakiwakosa baadhi ya wachezaji wao akiwepo Aziz Ki, Bangala na Bernad Morrison lakini nahodha wa klabu yao Mwamnyeto amesema pointi tatu ni muhimu.

Yanga na Ihefu Kusaka Pointi 3 Dimba la Mkapa.

Wakiwa kileleni na pointi zao 50 baada ya kucheza mechi 19 wanataka pia kutetea taji hili kwa mara ya pili mfululizo, lakini vijana kutoka Mbarali nao wanahitaji alama kuweza kutoka katika nafasi ya 13 waliyopo kwani sio nzuri.

Mchezo huo utapigwa kmajira ya saa 12:30 jioni ambapo tiketi zilishatoka mapema na viingilio vilishatajwa.

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.