Amiens Wapinga Kushushwa Daraja

Klabu ya Ligue 1, Amiens imetuma ombi “kudai haki” baada ya kushuka Daraja kutoka ligi kuu nchini Ufaransa kabla ya msimu kukamilika.

Paris St-Germain walipewa Ubingwa wa ligi siku ya Alhamisi huku Amiens na Toulouse wakishuka daraja baada ya serikali ya Ufaransa kufuta msimu wa michezo wa 2019-20 kwa sababu ya janga la coronavirus.

Amiens walikuwa nafasi ya 19 katika Msimamo wa Ligi, alama nne nyuma ya Nimes na alama 10 mbele ya Toulouse na michezo 10 iliyobaki kucheza.

“Amiens inajiandaa kutuma ombi la kudai haki kwa uamuzi huu muhimu ambao unapingana na mchezo wa haki,” ilisema taarifa.

Ombi hilo litakwenda kwa chombo kinachosimamia ligi, “Ligue de football Professionnel”, kufikiria tena uamuzi wake wa kuwashusha daraja Klabu hizo mbili na badala yake kucheza Ligue 1 na timu 22 badala ya 20 mnamo 2020-21.

Kuwa na timu 22 Kama wanavyotaka ni pamoja na Lorient na Lens, ambao wamepandishwa daraja kutoka Ligue 2..

15 Komentara

    Nasubiri kuona maamuzi ya pingamizi lao. Thanks meridian for information

    Jibu

    Madai yao ni kwel kabisa na pendekezo lao n zur maamuz ya busara yanahitajika

    Jibu

    yap..wanastahili kupata haki yao

    Jibu

    jaman wenye zaman ya ligue 1 haki na busara itendeke jaman

    Jibu

    Kweli watabadisha maamuzi ya awali , Mimi naona hiyo Ndio imeshapita washuke tu

    Jibu

    Tunasubir mamuz tu

    Jibu

    Wakubaliane na matokea

    Jibu

    Hili nilijua ya kuwa litatokea sababu kila mmoja anahisi kwa mechi zilizobaki anaweza jitetea

    Jibu

    Kusema kwamba maamuzi yalitolewa bila kushirikisha viongozi wa clubs?…asante meridianbettz kwa taarifa hizi

    Jibu

    Wakubali tu kama Wanatakiwa kushuka daraja washuke malumbano ayatakiwi kwenye mpira

    Jibu

    Wameonewa tu.

    Jibu

    haki itendeke

    Jibu

    Hapo ni haki tu na sio vinginevyo

    Jibu

    Haki inatakiwa hapo

    Jibu

    Dah pole yao

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.