Kiungo wa kimataifa wa Morocco anayekipiga kwa mkopo klabu ya Manchester United Sofyan Amrabat amesema vilabu kadhaa vilihitaji sana saini yake lakini kwake Man United ndio ilikua kipaumbele.
Amrabat ambaye ameanza katika kikosi cha Man United kwa mara ya kwanza jana katika ushindi wa mabao matatu kwa bila dhidi ya Palace, Ameweka wazi kua akili yake ilikua inaiwaza Man United.
Kiungo huyo ambaye dili lake lilikamilika siku ya mwisho ya usajili na hiyo ilitokana na yeye kuweka msimamo mgumu kua anataka kucheza Man United tu, Kwani kuna vilabu kadhaa vilimfata na klabu yake ya Fiorentina lakini kiungo huyo aliieleza klabu yake kua anataka kucheza Man United tu.
Kiungo huyo ameonesha uwezo mkubwa jana katika mchezo wa kombe la Carabao licha ya kuchezeshwa kama beki wa kushoto, Huku akisisitiza kua kucheza Manchester United ni ndoto yake tangu akiwa mdogo na sasa ndoto imetimia.
Kiungo Sofyan Amrabat baada ya kucheza mchezo wake wa jana mashabiki wa klabu hiyo wameonesha kuvutiwa na kiwango chake kwa kiwango kikubwa, Huku wakiamini ushirikiano wake na kiungo Casemiro katikati utakua na msaada sana kwa klabu hiyo.

