Klabu ya Arsenal inadaiwa kuwa imewasilisha ofa ya ufunguzi ya pauni milioni 17 kwa kiungo wa Lyon Houssem Aouar.
Washika bunduki wako sokoni la safu ya kati baada ya Dani Ceballos na Martin Odegaard kurejea Real Madrid, huku Granit Xhaka akiatarajiwa kuwafuata wawili hao pamoja na Matteo Guendouzi.
Aouar anaaminika alikuwa kwenye rada ya Arsenal kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, na kwa kuwa mkataba wake wa Lyon ulipaswa kumalizika mnamo 2023, uhamisho wake kwenda Emirates Stadium unakuwa na nafuu zaidi.

Kwa mujibu wa Le 10 Sport, Arsenal sasa wamewasiliana na Lyon na ofa ya pauni milioni 17 tayari imewasilishwa, lakini Lyon bado wana msimamo wa ada ya karibu na £ 21m.
Ripoti hiyo inaongeza kuwa Tottenham Hotspur wamejiandaa kupambana na wapinzani wao wa London Kaskazini kuipata saini ya Aouar, na kikosi cha Nuno Espirito Santo kitaweza kutoa ofa bora zaidi ya Washika bunduki.
Aouar alifunga mabao saba na kusaidia mengine matatu katika michezo 30 ya Ligue 1 muhula uliopita pale Lyon.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!



Ernest
Arsenal ikifeli tena msimu huu basi hawatompata tena
Sarah
Wajitahidi wampate