Mkuu wa klabu ya Juventus, Pavel Nedved amesema kuwa klabu haijapokea ombi wala kuona ishara yeyote ya nyota wao Christian Ronaldo kutaka kuondoka klabuni hapo.
Juventus hawakuwa na msimu mzuri chini meneja Andrea Pirlo kwa msimu wa 2020-21, wakishindwa kulinda taji lao dhidi ya Inter Milan, huku wakitolewa kwenye Ligi ya Mabingwa katika hatua ya mtoano wa timu 16 dhidi ya Porto.

Nyota huyo, ambaye kwa sasa y6upo likizo baada ya kumaliza majukumu ya kulitumikia taifa lake kwenye EURO2020, amekuwa akihusishwa sana na kuondoka klabuni hapo baada ya msimu mbaya kwa klabu hiyo.
Mkataba wa Ronaldo kusalia Turin umesalia chini ya miezi 12, na alikuwa akihusishwa zaidi na kurejea klabuni Manchester United, lakini dili hilo halionekani tena kuwa na msisitizo wakati United wakijiandaa kumtangaza rasmi Jadon Sancho.
Nyota huyu wa Ureno amefanya vyema kwenye michuano ya EURO 2020 na kuondoka na kiatu cha dhahabu akiwa na magoli matano na asisti moja kwenye mechi nne za Ureno. Alimaliza msimu wa Serie A akiwa na magoli 29 katika safari 33 za ligi.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!



Ernest
Itakuwa pouwa sana kama CR7 atasalia Juventus
Issa
Lazim abakie awape champion league